Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن الفحش وبذاء اللسان
074-Mlango Wa Kukatazwa Kutoa Maneno Machafu na ya Kishenzi
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن ابن مسعودٍ رضي الله عنه ، قال : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لَيْسَ المُؤْمِنُ بالطَّعَّانِ ، وَلاَ اللَّعَّانِ ، وَلاَ الفَاحِشِ ، وَلاَ البَذِيِّ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini hawi ni mwenye kusuta wala kulaani kutupa maneno machafu wala kutusi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 2
وعن أنسٍ رضي الله عنه قال : قالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَا كَانَ الفُحْشُ فِي شَيْءٍ إلاَّ شَانَهُ ، وَمَا كَانَ الحَيَاءُ فِي شَيْءٍ إلاَّ زَانَهُ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Utumiaji wa maneno machafu hauchang'anyiki na kitu chochote isipokuwa hukichafua. Na haya haiwi pamoja na kitu chochote isipokuwa hukirembehsa." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11394&title=074-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kutoa%20Maneno%20Machafu%20na%20ya%20Kishenzi