Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الالتفات في الصلاة لغير عذر
088-Mlango Wa Ukaraha wa Kugeuka Geuka katika Swalaah Bila Udhuru Wowote
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : سألت رسُولَ الله صلى الله عليه وسلم عَنِ الالتفَاتِ في الصَّلاَةِ ، فَقَالَ : (( هُوَ اخْتِلاَسٌ يَخْتَلِسُهُ الشَّيْطَانُ مِنْ صَلاَةِ العَبْدِ )) . رواه البخاري .
Amasema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu kugeuka (upande wa kulia na kushoto) katika Swalaah, akasema: "Kufanya hivyo ni udokozi anaodokoa shetani katika Swalaah ya mja." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن أنس رَضِيَ اللهُ عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إيَّاكَ والالتِفَاتَ فِي الصَّلاَةِ ، فَإنَّ الالتفَاتَ في الصَّلاَةِ هَلَكَةٌ ، فَإنْ كَانَ لاَ بُدَّ ، فَفِي التَّطَوُّعِ لاَ في الفَريضَةِ )) . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Jiepushe na kugeuka geuka katika Swalaah, kwani kugeuka katika Swalaah ni maangamivu. Ikiwa hapana budi mpaka ugeuke basi iwe sio katika Swalaah ya faradhi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11408&title=088-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kugeuka%20Geuka%20katika%20Swalaah%20Bila%20Udhuru%20Wowote