Hadiyth Al-Qudsiy
Hadiyth Ya 41
Jannah Na Moto Vilishindana Allaah Akahukumu Baina Yake
عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((احْتَجَّتْ الْجَنَّةُ وَالنَّارُ فَقَالَتْ النَّارُ: فِيَّ الْجَبَّارُونَ وَالْمُتَكَبِّرُونَ، وَقَالَتْ الْجَنَّةُ: فِيَّ ضُعَفَاءُ النَّاسِ وَمَسَاكِينُهُمْ، قَالَ: فَقَضَى بَيْنَهُمَا: إِنَّكِ الْجَنَّةُ رَحْمَتِي أَرْحَمُ بِكِ مَنْ أَشَاءُ، وَإِنَّكِ النَّارُ عَذَابِي أُعَذِّبُ بِكِ مَنْ أَشَاءُ، وَلِكِلَاكُمَا عَلَيَّ مِلْؤُهَا)) البخاري، مسلم و الترمذي
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jannah na moto vilishindana. Moto ulisema: Ndani yangu wamo wenye kujifanya majabari na wenye kutakabari. Jannah ikasema: Ndani yangu wamo watu dhaifu na maskini. Akasema: Allaah Akahukumu baina yao: (Akasema): Wewe Jannah ni rahmah Zangu, kupitia kwako wewe Humrehemu Nimtakaye. Nawe moto ni adhabu Yangu, kupitia kwako wewe ninawaadhibu wale niwatakao na kila mmoja katika nyinyi mtajaa)) [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F2696&title=41-Hadiyth%20Al-Qudsiy%3A%20Jannah%20Na%20Moto%20Vilishindana%20Allaah%20Akahukumu%20Baina%20Yake