Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu
Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.
Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com [1]
05-Kwanini Allaah Ametuma Rusuli?
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amewatuma Rusuli ili walinganie watu kumwabudu na kuepukana na kumshirikisha.
وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ ۖ
Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Rasuli (alinganie) kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na twaghuti. [An-Nahl: 36]
((الأنبياء إخوةٌ ودينُهُم واحد)) متّفق عَلَيهِ
أَيْ كلُّ الرسل دعوا إِلَى التّوحيد
((Manabiy ni ndugu na Dini yao ni moja)) [Al-Bukhaariy, Muslim]
Yaani: Rusuli wote wamelingania Tawhiyd
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7739&title=05-Mukhtasari%20Aqiydah%20Ya%20Muislamu%3A%20Kwanini%20Allaah%20Ametuma%20Rusuli%3F