Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu
Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.
Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com [1]
09-Nini faida ya Tawhiyd kwa Muislamu?
Faida ya Tawhiyd kwa Muislamu ni kupata Hidaaya duniani na kuwa katika amani Aakhirah.
الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ أُولَـٰئِكَ لَهُمُ الْأَمْنُ وَهُم مُّهْتَدُونَ ﴿٨٢﴾
Wale walioamini na hawakuchanganya iymaan zao na dhulma; hao ndio watakaopata amani nao ndio walioongoka. [Al-An’aam: 82]
((وَحَقُّ الْعِبَادِ عَلى اللهِ أَنْ لاَ يُعَذِّبَ مَنْ لاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا)) متّفق عَلَيهِ
((Haki ya waja kwa Allaah ni kwamba Hatomwadhibu yeyote ambaye hamshirikishi na chochote kile)) [Al-Bukhaariy, Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7765&title=09-Mukhtasari%20Aqiydah%20Ya%20Muislamu%3A%20Nini%20faida%20ya%20Tawhiyd%20kwa%20Muislamu%3F