Mlango Wa 45
بَابٌ مَنْ سَبَّ الدَّهْرَ فَقَدْ آذَى اللَّهَ
Anayetukana Wakati Amemuudhi Allaah
وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:
Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:
وَقَالُوا مَا هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا الدُّنْيَا نَمُوتُ وَنَحْيَا وَمَا يُهْلِكُنَا إِلَّا الدَّهْرُ ۚ وَمَا لَهُم بِذَٰلِكَ مِنْ عِلْمٍ ۖ إِنْ هُمْ إِلَّا يَظُنُّونَ ﴿٢٤﴾
((Na wakasema: “Huu si chochote isipokuwa ni uhai wetu wa dunia, tunakufa na tunahuika, na hakuna cha kutuangamiza isipokuwa zama tu.” Na wala hawana kwayo ujuzi wowote, ila wao wanadhania tu)) [Al-Jaathiyah (45: 24)]
وَفِي الصَّحِيحِ: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنِ النَّبِيِّ (صَلَى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((قَالَ اللَّهُ تَعَالَى: يُؤْذِينِي ابْنُ آدَمَ يَسُبُّ الدَّهْرَ، وَأَنَا الدَّهْرُ أُقَلِّبُ الْلَّيْلَ وَالنَّهَارَ))
Na katika Swahiyh, Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Ta’aalaa Amesema: Bin Aadam ananiudhi, kwani anatukana dahari [wakati au zama], na hali Mimi ni Ad-Dahr [Namiliki kila kitu na uwezo], Nageuza usiku na mchana)).
وَفِي رِوَايَةٍ: ((لا تَسُبُّوا الدَّهْرَ؛ فِإنَّ اللَّهَ هُوَ الدَّهْرُ))
Na katika riwaayah: ((Msitukane dahari kwani hakika Allaah ni Ad-Dahr)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Masuala Muhimu Yaliyomo:
1-Kulaani wakati kumekatazwa.
2-Kutukana wakati ni kumkosoa Allaah (سبحانه وتعالى).
3-Kutafakari kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Hakika Allaah ni Ad-Dahr)).
4-Jambo linaweza kuwa tusi hata kama haliko katika hisia (za mtukanaji).
Links
[1] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7901&title=45-Kitaab%20At-Tawhiyd%3A%20Anayetukana%20Wakati%20Amemuudhi%20Allaah