Aayah Na Mafunzo
Aal-‘Imraan
Unyenyekevu Wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Kutaka Ushauri Kwa Swahaba
Alhidaaya.com [1]
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
فَبِمَا رَحْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ لِنتَ لَهُمْ ۖ وَلَوْ كُنتَ فَظًّا غَلِيظَ الْقَلْبِ لَانفَضُّوا مِنْ حَوْلِكَ ۖ فَاعْفُ عَنْهُمْ وَاسْتَغْفِرْ لَهُمْ وَشَاوِرْهُمْ فِي الْأَمْرِ ۖ فَإِذَا عَزَمْتَ فَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚإِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُتَوكِّلِينَ ﴿١٥٩﴾
Basi ni kwa rahmah kutoka kwa Allaah umekuwa mpole kwao (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم). Na lau ungelikuwa mjeuri mwenye moyo mgumu wangelitawanyika mbali nawe. Basi wasamehe na waombee maghfirah na washauri katika mambo. Na unapoazimia basi tawakali kwa Allaah. Hakika Allaah Anapenda wanaotawakali. [Aal-'Imraan: 159]
Mafunzo:
Upole na unyenyekevu wa Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) umetajwa mare tele katika Qur-aan na Sunnah, na rejea Aayah (9: 128).
Amri na pendekezo la kutafuta ushauri: Allaah (سبحانه وتعالى) Amemuamrisha Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) atake ushauri kwa Swahaba zake, naye (صلى الله عليه وآله وسلم) akawataka wamshauri katika hali kadhaa ili awatulize nyoyo zao. Na hili ni funzo kwamba ushauri ni jambo muhimu na pia mkubwa au mwenye cheo anaweza kutafuta ushauri kwa wadogo wake au walio duni yake.
Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliwataka ushauri Swahaba zake katika mambo mbali mbali, mfano;
Na katika hali nyinginezo mbalimbali alikuwa akiwataka ushauri Swahaba zake (رضي الله عنهم).
Kwa faida ziyada tafadhali bonyeza kiungo kifuatacho:
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/sw
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/node/10189
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8158&title=159-Aayah%20Na%20Mafunzo%3A%20Unyenyekevu%20Wa%20Nabiy%20%28%D8%B5%D9%84%D9%89%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%20%D8%B9%D9%84%D9%8A%D9%87%20%D9%88%D8%A2%D9%84%D9%87%20%D9%88%D8%B3%D9%84%D9%85%29%20Kutaka%20Ushauri%20Kwa%20Swahaba%20