Akiwa Ndani Ya Ihraam Amechezea Nywele Kisha Zimeng'oka
Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)
SWALI:
Nina tabia ya kuchezea nywele ninapoikuwa na fikra. Nilipokwishaingia katika ihraam, bila ya kujitambua, nilifanya hivyo na baadhi ya nywele ziling'oka na kuanguka. Je, napaswa kulipa kafara?
JIBU:
Hakuna haja kufanya hivyo (kulipa kafara) kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametaja kuhusu Waumini kwamba wamesema:
رَبَّنَا لاَ تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا
“Rabb wetu Usituchukulie tukisahau au tukikosea. [Al-Baqarah:286]
Kisha Allaah Akawajibu du'aa yao hii kama ilivyotajwa katika Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Aliitikia kwa kusema:
((قَدْ فَعَلْت))
(Nimeiitikia [du'aa]) [Muslim katika Swahiyh yake]
[Fataawa Al-Hajj Wal 'Umrah waz-Ziyaarah Uk. 58]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9225&title=01-Imaam%20Ibn%20Baaz%3A%20Akiwa%20Ndani%20Ya%20Ihraam%20Amechezea%20Nywele%20Kisha%20Zimeng%27oka