Tarehe Ya Hijriy

Kibainisho Muhimu

Nasiha Na Ukumbusho: Swawm Tarehe 9 Na 10 Al-Muharram Inafuta Madhambi Ya Mwaka Mzima!

 

 

Nasiha Na Ukumbusho Wa Swawm

Siku Ya Taasu'aa (9) Na 'Aashuraa (10)

 

 Alhidaaya.com

 

  

Nasiha: Swiyaam Tarehe 9 na 10 Al-Muharram zimesisitizwa na fadhila zake  ni kufutiwa madhambi ya mwaka mzima kwa dalili kauli ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

((صِيَامُ يَوم عاشوراء إنِّي أحْتَسبُ علَى اللهِ أن يُكفِّرَ السَّنةَ التِي قبلَه)) رواه مسلم

"Swawm ya siku ya 'Ashuraa, nategemea kutoka kwa Allaah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia." [Muslim]

 

 

Asiyejaaliwa  kufunga tarehe 9 basi asikose Swawm ya tarehe 10 Al-Muharram pekee.

 

Bonyeza viungo vifuatavyo upate faida tele kuhusiana na Fadhila Za Mwezi wa Al-Muharram na Swiyaam zake:

 

 

Hukmu Ya Swawm Ijumaa Ikiwa Ni Siku Ya 'Arafah Au 'Aashuraa

 

 

Ukumbusho Wa Kukithirisha Swawm Mwezi wa Al-Muharram Na Swiyaam Ya Taasu'aa na 'Aashuraa (9 na 10 Al-Muharram) Pamoja Na Masiku Mengineyo)

 

 

Fadhila Za Mwezi Wa Al-Muharam Na Siku Ya 'Aashuraa Na Bid'ah Zake

 

 

Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah

 

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq

 

Share

Fadhila Za Mwezi Wa Al-Muharram, Siku Ya 'Aashuraa Na Bid'ah Zake

 

Fadhila Za Mwezi Wa Al-Muharram, Siku Ya 'Aashuraa Na Bid'ah Zake

Alhidaaya.com

 

 

AlhamduliLLaah, Tunamshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaaa) Kutufikisha tena katika mwaka mwengine mpya wa Kiislamu. Mwezi wa Al-Muharram una fadhila makhsusi kulingana na miezi mitukufu mingineyo. Moja wa fadhila hizo ni funga ya tarehe 9 na 10 Al-Muharram zinazojulikana kama Taasu'aa na 'Aashuraa. Hivyo ndugu Waislamu tusiache kufunga siku hizi mbili kwani thawabu zake ni kufutiwa madhambo ya mwaka mzima!

 

 قال النبي صلى الله عليه وسلم: ((صِيامُ يَوْمِ عَاشُورَاءَ أَحْتَسِبُ عَلَى اللَّهِ أَنْ يُكَفِّرَ السَّنَةَ الَّتِي قَبْلَهُ))  رواه مسلم

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swawm ya  siku ya 'Aashuraa, nataraji kutoka kwa Allaah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia)) [Muslim]

 

Bonyeza viungo vifuatavyo:

 

Ukumbusho Wa Kukithirisha Swawm Mwezi wa Al-Muharram Na Swiyaam Ya Taasu'aa na 'Aashuraa (9 na 10 Al-Muharram Pamoja Na Masiku Mengineyo)

 

 

Nasiha Na Ukumbusho Wa Swawm  Siku Ya Taasu'aa (9) Na 'Aashuraa (10)

 

 

Imaam Ibn Baaz: Lini Huanza Swawm Za Mwezi Wa Al-Muharram Na Je Siku Ngapi Za Swiyaam?

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Swiyaam Za Al-Muharaam Ni Kufunga Mwezi Mzima? Au Nitakuwa Nimezusha?

 

 

Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah

 

01-Al-Muharram: Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ﴿٣٦﴾

Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah, (tangu) siku Aliyoumba mbingu na ardhi. Kati ya hiyo, (iko miezi) minne mitukufu. Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu. Basi msijidhulumu humo nafsi zenu (kwa kufanya maasi), na piganeni vita na washirikina wote kama wao wanavyokupigeni vita nyote. Na jueni kwamba Allaah Yu Pamoja na wenye taqwa. [At-Tawbah: 36]

 

Na Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema katika Hadiyth:

 

عن أبي بَكْرَةَ رضي الله عنه عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أنه قَالَ:  إن الزَّمَانَ قَدْ اسْتَدَارَ كَهَيْئَتِهِ يَوْمَ خَلَقَ اللَّهُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ السَّنَةُ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ثَلاثٌ مُتَوَالِيَاتٌ ذُو الْقَعْدَةِ وَذُو الْحِجَّةِ وَالْمُحَرَّمُ وَرَجَبُ مُضَرَ الَّذِي بَيْنَ جُمَادَى وَشَعْبَانَ

Imepokelewa kutoka kwa Abu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika mgawano wa zama umerudi katika hali yake ya asili siku Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Mwaka una miezi kumi na mbili; minne miongoni ya hiyo ni mitukufu, mitatu inafuatana pamoja; Dhul-Qa'adah, Dhul-Hijjah na Al-Muharram, mwengine ni Rajab wa (kabila la) Mudhwarr ambao uko baina ya Jumaadaa na Sha'baan))  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Faida Kuhusu Mwezi Wa Al-Muharram

 

1-Swawm (funga) yake ni swawm bora kabisa baada ya Ramadhwaan:

 

Bonyeza Endelea...

 

 

 

Share

Ukumbusho Wa Kukithirisha Swawm Mwezi wa Al-Muharram Na Swiyaam Ya Taasu'aa na 'Aashuraa (9 na 10 Al-Muharram) Pamoja Na Masiku Mengineyo

 

 Al-Muharram 

Ukumbusho Wa Kukithirisha Swiyaam (Funga) Za Mwezi wa Al-Muharram

Na Swiyaam Ya Taasu'aa na 'Aashuraa  (9 na 10 - Al-Muharram) Pamoja Na Masiku Mengineyo 

Alhidaaya.com

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: 

 أَفْضَلُ الصِّيَامِ بَعْدَ رَمَضَانَ شَهْرُ اللَّهِ الْمُحَرَّمُ  رواه مسلم

"Swiyaam (funga) bora kabisa baada ya Ramadhwaan ni swawm ya mwezi wa Allaah wa Al-Muharram." [Muslim]

 

Tunawanasihi hali kadhalika kufunga siku ya Taasu'aa na 'Aashuraa (Tarehe 9 na 10 Al-Muharram). Asiyeweza Swawm tarehe 9 Al-Muharram basi baadhi ya 'Ulamaa wanasema kuwa mtu anaweza kufunga tarehe 10 na 11 Al-Muharram japokuwa hakuna Hadiyth sahihi ya kufunga siku ya baada yake; yaani Al-Muharram 11. Na asiyejaaliwa kuunganisha Swawm tarehe 9 pamoja na tarehe 10 au kuunganisha Swawm tarehe 10 pamoja na 11 Al-Muharram, basi asikose Swawm ya tarehe 10 Al-Muharram pekee. Hayo ni kutokana na fadhila zake za kufutiwa madhambi ya mwaka mmoja kama ilivyothibiti katika Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

((صِيَامُ يَوم عاشوراء إنِّي أحْتَسبُ علَى اللهِ أن يُكفِّرَ السَّنةَ التِي قبلَه)) رواه مسلم

"Swawm ya siku ya 'Ashuraa, nategemea kutoka kwa Allaah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia." [Muslim]

 

Kwa faida zaidi soma makala katika kiungo kifuatacho:

 

Fadhila Za Mwezi Wa Al-Muharam Na Siku Ya 'Aashuraa Na Bid'ah Zake

 

Masiku mengineyo ya Swiyaam za Sunnah na fadhila zake:

 

Jumatatu na Alkhamiys:    

 

عن أبي هريرة رضي الله عنه: تُعرَضُ الأعمالُ يومَ الاثنينِ والخميسِ فأحبُّ أن يُعرَضَ عملي وأنا صائمٌ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “'Amali zinapandishwa siku ya Jumatatu na Alkhamiys, basi napenda kwamba zipandishwe 'amali zangu nikiwa mimi niko katika Swawm.” [Swahiyh At-Tirmidhiy 747, Swahiyh At-Targhiyb 1041]

 

Swiyaam ya Jumatatu:

 

عَنْ أَبِي قَتَادَةَ الْأَنْصَارِيِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سُئِلَ عَنْ صَوْمِ الِاثْنَيْنِ فَقَالَ: (( فِيهِ وُلِدْتُ وَفِيهِ أُنْزِلَ عَلَيَّ)) .

Kutoka kwa Abuu Qataadah Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu Swawm ya Jumatatu akasema: “Nimezaliwa siku hiyo na siku hiyo nimeteremshiwa (Qur-aan).” [Muslim]

 

 

Ayyaamul-Biydhw (Tarehe 13, 14, 15)

 

 

Swawm Ya Nabiy Daawuwd:  Siku Kufunga Na Siku Kuacha kutokana na Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

أَحَبُّ الصِّيَامِ إِلَى اللَّهِ صِيَامُ دَاوُدَ، كَانَ يَصُومُ يَوْمًا وَيُفْطِرُ يَوْمًا

"Swawm inayopendeza zaidi kwa Allaah ni Swawm ya Daawuwd, alikuwa anafunga siku moja na anakula siku moja” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida za fadhila za Swiyaam:

 

Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah

 

 

Tutaweka taarifa za kuandama mwezi In Shaa Allaah.  

 

 

Share

01-Al-Muharram: Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

 

01-Al-Muharram

 

Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

 

 

Alhidaaya.com

 

 

Ukumbusho Wa Kukithirisha Swawm Mwezi wa Al-Muharram Na Swiyaam Ya Taasu'aa na 'Aashuraa (9 na 10 Al-Muharram Pamoja Na Masiku Mengineyo)

 

 

Nasiha Na Ukumbusho Wa Swawm  Siku Ya Taasu'aa (9) Na 'Aashuraa (10)

 

 

Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah

 

 

 

 

Fadhila Za Mwezi Wa Al-Muharram, Siku Ya 'Aashuraa Na Bid'ah Zake

 

 

 

 

 

Imaam Ibn Baaz: Lini Huanza Swawm Za Mwezi Wa Al-Muharram Na Je Siku Ngapi Za Swiyaam?

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Aanze Kufunga Swiyaam Za Sunnah Kama ‘Aashuraa Kwanza Au Alipe Swiyaam Za Kuwajibika Kama Ramadhwaan?

 

 Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Swiyaam Za Al-Muharaam Ni Kufunga Mwezi Mzima? Au Nitakuwa Nimezusha?

 

Al-Lajnah Ad-Daa'imah: Hairuhusiwi Kupongezana Kwa Mnasaba Wa Mwaka Mpya Wa Hijri (Kiislamu) Au Maulidi

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Aashuraa: Bid’ah Zake: Kuwachinjia Maiti, Mikusanyiko Ya Visomo

  

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Aashuraa: Kulipa Deni La Siwyaam Za Ramadhwaan Na ‘Aashuraa

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Aashuraa: Swawm Siku Moja Ya ‘Aashuraa Pekee Inajuzu?

 

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Aashuraa: Kuchinja Siku Ya ‘Aashuraa Imo Katika Shariy'ah?

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Aashuraa: Kinachowajibika Siku Ya 'Aashuraa Je Inawajibika Zakaatul-Fitwr?

 

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Miongoni Mwa Bid’ah Za ‘Aashurah Ni Kuchinja Kwa Ajili Ya Waliofariki Na Kukusanyika Kusoma Qur-aan

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Mwenye Hedhi Siku Ya 'Aashuraa Je Inajuzu Alipe Swawm Hiyo? Nini Hukmu Ya Kulipa Nawaafil?

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Aashuraa: Aanze Swiyaam Za ‘Aashuraa Au Alipe Swiyaam Za Ramadhwaan?

 

 Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Aashuraa: Inafaa Swawm Siku Ya ‘Aashuraa Pekee Au Ni Makruwh (Inachukiza)?

 

 Imaam Ibn Baaz: Al-Muharram: Lini Huanza Swawm Za Al-Muharram Na Je Siku Ngapi Za Swiyaam?

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Swiyaam Za Al-Muharaam Ni Kufunga Mwezi Mzima? Au Nitakuwa Nimezusha?

 

 

 

Imaam Ibn Rajab - Kunasibishwa Mwezi Wa Al-Muharram Na Allaah

 

 

 

 

 

Mafunzo Kutoka Katika Hijrah -- Siyrah Ya Nabiy

 

Mashairi: Mwaka Mpya Wa Kiislamu -- Mashairi

 

Al-Husayn Bin 'Aliy (Radhiya Allaahu 'anhuma) -- Swahaaba

 

Mwaka Mpya Wa Kiislamu Na Hukumu Ya Kusherehekea -- Bidah-Uzushi

 

Swawm Ya ‘Ashuraa Baina Ya Wenye Kupinga Na Wenye Kuunga Mkono – Makundi Potofu

 

Hijrah: Chanzo Cha Mageuzi -- Siyrah Ya Nabiy

 

 

 

 

 

 

Uzushi Unaodaiwa Kuhusu Mambo Yaliyotokea Siku Ya 'Aashuraa Tarehe 10 -- Maswali: Bid'ah - Uzushi

 

Hukmu Ya Swawm Ijumaa Ikiwa Ni Siku Ya 'Arafah Au 'Aashuraa

 

Kufunga Swawm Za Sunnah Kuanzia Ijumaa Inafaa?

 

Orodha Ya Majina Ya Miezi Ya Kiislaam (Hijri) -- Maswali: Taariykh

 

Tofauti Ya Miezi Ya Kiislamu (Hijriyyah) Na Ya Miladi Zipi Sifa Zake? -- Maswali: Mchanganyiko

 

 

Miezi Ya Kiislamu Na Makosa Yaliyozooleka Katika Jamii Kwa Kuitaja Kwa "Mfungo Kadhaa" -- Maswali: Siyrah

 

Uzushi Kuhusu Swalah Maaulum Ya Jumatano Ya Mwisho Mfungo Tano (Swafar)

 

 

Share

Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

'Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

 

Alhidaaya.com

 

 

AlhamduliLLaah. Inapasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Kutuendeleza uhai katika mwezi mwengine mtukufu.  Ni fursa nyingine ya kutenda mema tuchume thawabu nyingi. Mema ambayo hatuna budi kuyatenda kwa ajili ya kujenga Aakhirah yetu kabla haijafika siku ya kuaga kwetu dunia.

 

Utukufu wa miezi hiyo mitukufu imetajwa katika Qur-aan na Sunnah: Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ﴿٣٦﴾

Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah, (tangu) siku Aliyoumba mbingu na ardhi. Kati ya hiyo, (iko miezi) minne mitukufu. Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu. Basi msijidhulumu humo nafsi zenu (kwa kufanya maasi), na piganeni vita na washirikina wote kama wao wanavyokupigeni vita nyote. Na jueni kwamba Allaah Yu Pamoja na wenye taqwa. [At-Tawbah: 36]

 

Na miezi hiyo minne mitukufu imetajwa katika Hadiyth ifuatayo:

 

عن أبي بَكْرَةَ رضي الله عنه عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أنه قَالَ:  ((إن الزَّمَانَ قَدْ اسْتَدَارَ كَهَيْئَتِهِ يَوْمَ خَلَقَ اللَّهُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ السَّنَةُ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ثَلاثٌ مُتَوَالِيَاتٌ ذُو الْقَعْدَةِ وَذُو الْحِجَّةِ وَالْمُحَرَّمُ وَرَجَبُ مُضَرَ الَّذِي بَيْنَ جُمَادَى وَشَعْبَانَ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika mgawano wa zama umerudi katika hali yake ya asili siku Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Mwaka una miezi kumi na mbili; minne miongoni ya hiyo ni mitukufu, mitatu inafuatana pamoja; Dhul-Qa'adah, Dhul-Hijjah na Muharram, mwengine ni Rajab wa (kabila la) Mudhwarr ambao uko baina ya Jumaadaa na Sha'baan))  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Imaam Atw-Twabariy amesema:

 

 

Share