51-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kutoa sadaka mali ambayo haikuusiwa
Kutoa sadaka mali ambayo haikuusiwa:
Muslim amepokea kuwa: kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam), ‘Baba yangu amefariki na ameacha mali ambayo hakuusia chochote; Je, nikitoa sadaka mali hiyo itamsaidia kumpunguzia madhambi yake au je, atapata malipo kwa jambo hilo? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akajibu, “Ndiyo.”
