09-Uswuul Al-Fiqhi: Kipindi Cha Maswahaba Wakuu
Baada ya kipindi cha Mbora wa Mitume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), ukaingia wakati wa Maswahaba wakuu na viongozi walioongoka vyema Khulafau’ ar-Raashiduun. Kipindi hichi kilidumu kutoka mwaka 11 hadi 40 A.H. Wasomaji Qurra’ ni neno lililokuwa linatumika wakati huu kumaanisha wale Swaababah wenye utambuzi mzuri wa Fiqhi na waliokuwa wakitoa Fatawa.
