35-Mukhtasari Aqiydah Ya Muislamu: Je, Inajuzu kutundika au kuvaa hirizi?
Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu
Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.
Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com
35-Je, Inajuzu kutundika au kuvaa hirizi?
Hapana! Haijuzu kutundika au kuvaa hirzi kwa sababu ni shirki.
وَإِن يَمْسَسْكَ اللَّـهُ بِضُرٍّ فَلَا كَاشِفَ لَهُ إِلَّا هُوَ ۖ
Na Allaah Akikugusisha kwa dhara, basi hakuna yeyote wa kukuondolea hiyo isipokuwa Yeye [Al-An’aam: 17]
((من علّق تميمةً فَقَدْ اشرك)) صحيح رواه أحمد
((Atakayetundika hirizi, atakuwa ameshirikisha Allaah)) [Hadiyth Swahiyh ameipokea Ahmad]
