Basbusa 1 (Shaam)

 Basbusa 1 (Shaam)

 

Vipimo                                             

Unga wa Semolina -  2 Vikombe

Nazi ya chenga 1 kikombe

Siagi (butter) au samli -   3/4  kikombe

Sukari - 3/4  kikombe

Mtindi (Yoghurt au buttermilk) -  1 1/4 kikombe

Vanila-    1-2 kijiko cha chai

Baking powder  - 1 kijiko cha chai

Baking soda- 1 1/2 kijiko cha chai

Lozi zilizomenywa maganda kwa ajili ya kupambia. 

Shira

Sukari  - 1 kikombe

Maji  - 1 kikombe

Ndimu ya maji - 1 kijiko cha chai

Pika shira mapema. Chemsha kwa muda wa dakika 20-25 itakapopoa  iwe nzito kidogo sio nyepesi sana.  

Namna Ya Kutayarusha Na Kupika

  1. Washa oveni moto wa 350ºF
  2. Yayusha siagi au samli na iache ipowe.
  3. Changanya sukari na mtindi katika bakuli kubwa.
  4. Changanya semolina, nazi, vanila, baking powder, baking soda katika bakuli jengine.
  5. Tia mchanganyiko wa semolina katika bakuli lenye mchanganyiko wa sukari na mtindi na changanya vizuri.
  6. Paka siagi katika sinia ya oveni (baking tray) ya saizi 11" x 7 " au 13" x 9" na tandaza mchanganyiko.
  7. Weka alama ya kukata vipande vipande vya mraba (square) na katika kila kipande weka lozi moja juu yake kupambia.
  8. Iache kwa muda wa dakika 15-20 kabla ya kuipika.
  9. Pika (bake) kwa muda wa dakika 30 au zaidi kidogo hadi iwive na igeuke rangi.
  10. Epua katika oveni na mwagia shira wakati bado imoto na shira iwe iliyopoa baridi.

Kidokezo:

Ikiwa basbusa ni imoto  basi shira iwe baridi, na ikiwa basbusa ni ibaridi basi shira iwe imoto.

 

Share