Pudini Ya Mayai Kwa Karameli

Pudini Ya Mayai Kwa Karameli


 

Vipimo:

Maziwa - 2 ½ mugs

Mayai - 8

Sukari - 1 kikombe cha chai

Illiki - ½ kijiko cha chai

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Unatia mayai yote 8 kwenye blender,maziwa ,hiliki na sukari robo kikombe ikisha unasaga kwa dakika 3.
  2. Sukari iliyobaki unaitia kwenye sufuria moto mdogo mdogo unaiyayusha mpaka iyayuke na iwe brown,unaiwacha kidogo ikisha unaisambaza kwenye sufuria    humo humo. Mpaka ienee nusu ya sufuria lako.
  3. Chukuwa mchanganyiko wa maziwa na mayai umimine humo kwenye sufuria la sukari iliyoyayushwa halafu funika.
  4. Chukuwa sufuria nyingine kubwa ya hiyo uliyotilia sukari na mchanganyiko ikisha itie maji nusu na uiteleke ndani yake tia sufuria yako yenye pudding.kumbuka sufuria ya pudding itakuwa inaelea kwahiyo tafute kitu kizoto ukiweke juu ya sufuria ya ndani yenye pudding.
  5. Iache itokote mpaka maji yakianza kumalizika ongeza maji mengine ,huku unaifunguwa kuitizama ukiona tayari imeshaganda yaani imeshajishika basi iepuwe wacha ipowe.
  6. Ikipowa mimina kwenye chombo kama sahani yenye shimo kidogo ikisha weka ndani ya fridge, ikishapata ubaridi tayari kwa kuliwa.

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kuburudika)

 

 

 

Share