Uzushi Wa Swalah Za Usiku

 

 

Uzushi Wa Swalah Za Usiku

 

Alhidaaya.com

 

 

Assalaamualaykum   Ndugu   Zangu,

 

Mimi Siku Zote   Naamka Saa Nane  Za Usiku  ---  Yaani Na Amshwa Naturally.

 

Nina Sali Kwa Mpango   Ufuatao:

 

I.       Sunnatil-udhuu       Rakaa 2

II.      Sunnati    Rasulullah (s.a.w.)   Rakaa   2

III.     Thajjud    Rakaa    2

IV.     Sunna Ya Usiku Ule Raka ....kama Ilvyoandikwa

V.      Sunnati   Hajjat Rakaa 2 ,2,2, Mujibu Wa Haja Zangu.

VI.     

Sunnati   Tawba    Rakaa 2

VII.   Salaatul  Witr     Rakaa   3.

 

 

By The Time   Nimewahi Zote   Swalah Ya Fajr   Ni Tayari.  Na Endelea  Kufanya  Zikrullah  Baada Ya Swalah  Ya Fajr   Mpaka Time Ya   Ishraaq    Na Tena   Naendelea Kuwepo  Kwenye  Msala Kwa Zikrullah Mpaka   Swalah Ya Dhuhaa.

 

 Jee    Ni Fafanulieni   Wapi Nimekosea Na Nifanye Sahihi Namna   Gani

 

 Jazaakallahukheir        Fiiamaanillah

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

 

Hakika hili ni jambo muhimu sana kwa kila Muislamu kwani katika kufanya ibada yoyote ikiwa ya vitendo au kauli,  lazima masharti mawili yapatikane ndipo ibada hiyo ikubaliwe nayo ni:

 

 

1)     Ikhlaas – Iwe kwa kutaka Ridhaa ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)  na sio yenye Riyaa au sio yenye kutendeka kwa ajili ya maslahi ya kidunia.

2)     Iwe inatokana na mafundisho ya Qur-aan na Sunnah. (kufanyika kwa mujibu wa mafunzo ya Qur-aan na Sunna sahihi).

 

 

Bila ya shaka sharti la kwanza dada yetu na wengi wetu tunalitimiza. Ama sharti la pili ndio baadhi yetu hatukulitambua ndipo tunapofanya ibada bila ya kupata dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah.

 

 

Tunakutajia hapa zilizo sahihi na zisizo sahihi kutokana na maelezo yako:

 

Swalaah

Daraja Yake

Dalili/Maelezo

 

Sunnatul- Wudhuu  Rakaa mbili 

sahihi

Dalili kuwa Bilaal (Radhwiya Allahu 'anhu) akiswali hata Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaota nyao zake zinatembmea Peponi kutekelza Swalaah hii kila baaya wudhuu.

Sunnatul-Rasuul   (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

sio sahihi

Hakuna dalili yoyote.

Tahajjud Rakaa 2

sahihi

Unaweza kuswali mbili, au nne, au sita au nane ukamalizia na tatu za Witr

 

Sunnah ya usiku

sahih

Ni sawa na Tahajjud usiongeze zaidi ya hizo

Sunnah ya Haja

dhaifu

Imepingwa na Maulamaa kuwa ni Hadiyth dhaifu. Muislamu anaomba haja zake kwa kuomba du'aa kama kawaida.

Sunnah ya  Tawbah

sahihi

Anapofanya mja dhambi anaswali Rakaa mbili kuomba maghfira

Salaatul Witr

sahihi

Rakaa 3 unamalizia baada ya kuswali 8 au chini yake za Tahajjud

 

 

Unavyomalizia kuwa inafika Alfajiri kisha unaendelea kufanya dhikru-Allah hadi litoke jua kisha unaswali Swalah ya Dhuhaa ni sawa kabisa na fadhila zake ni kupata thawabu kama vile umetimiza Hajj na Umra kamili kutona na Hadiyth ifuatayo:

 

((عن أنس عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنه قال : من صلى الفجر في جماعة ثم قعد يذكر الله  حتى تطلع الشمس ثم صلى ركعتين كانت له كأجر حجة وعمرة تامة تامة تامة) ) أخرج الترمذي  صححه الألباني .

Imetoka kwa Anas kwamba   Nabiy   (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayeswali Alfajiri katika Jama'ah kisha akakaa anamkumbuka Allaah mpaka likachomoza jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio kamili kamili kamili)) [Imetolewa na At-Tirmidhy na kaisahihisha Al-Albaaniy]

 

 

Tanbihi:  Fadhila hizi anazipata pia mwanamke sawa sawa atakaposwali nyumbani kwake. Tunakuombe dada yetu Allaah Azidi kukuelimisha upate kuona yaliyo haki uyafuate na ujiepushe na mambo ya uzushi yote.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

 

Share