053-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Uharamu wa Kufuga Mbwa Ila kwa Kuwinda au kwa Kulinda Wanyama au Mazao

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب تحريم اتخاذ الكلب إلا لصيد أو ماشية أو زرع

053-Mlango Wa Uharamu wa Kufuga Mbwa Ila kwa Kuwinda au kwa Kulinda Wanyama au Mazao

 

Alhidaaya.com

 

Hadiyth – 1

عن ابن عمر رضي الله عنهما، قال : سمعتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( مَنِ اقْتَنَى كَلْباً إلاَّ كَلْبَ صَيْدٍ أوْ مَاشِيَةٍ فَإنَّهُ يَنْقُصُ مِنْ أجْرِهِ كُلَّ يَومٍ قِيرَاطَانِ )) . متفق عليه .

وفي رواية : (( قِيرَاطٌ )) .

Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kuweka mbwa asiekuwa wa kuwinda au wa kulinda mali na mifugo (kama ngamia, kondoo na mbuzi), hakika thawabu zake kila siku Qiyraat mbili." [Al-Bikhaariy na Muslim].

Na katika riwaayah nyengine: "Qiyraat moja."

 

Hadiyth – 2

وعن أبي هريرة رضي الله عنه قال : قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ أمْسَكَ كَلْباً، فَإنَّهُ ينْقُصُ مِنْ عَمَلِهِ كُلَّ يَومٍ قِيرَاطٌ إلاَّ كَلْبَ حَرْثٍ أوْ مَاشِيَةٍ )) . متفق عليه .

وفي رواية لمسلم : (( مَنْ اقْتَنَى كَلْباً لَيْسَ بِكَلْبِ صَيْدٍ، وَلاَ مَاشِيَةٍ وَلاَ أرْضٍ، فَإنَّهُ يَنْقُصُ مِنْ أجْرِهِ قِيرَاطَانِ كُلَّ يَوْمٍ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Atakaye kuwa na mbwa, hakika yeye anapungukiwa kila siku na Qiyraat moja ya amali zake isipokuwa mbwa wa kulinda mazao au wanyama." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na katika riwaayah ya Muslim: "Mwenye kumueka mbwa ambaye si wa kuwinda wala wa kulinda ardhi, hakika atapungukiwa katika ajri yake Qiyraat mbili kila siku." 

 

 

Share