087-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kukatazwa Kunyanyua Macho Juu Mbinguni katika Swalaah

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب النهي عن رفع البصر إِلَى السماء في الصلاة

087-Mlango Wa Kukatazwa Kunyanyua Macho Juu Mbinguni katika Swalaah

 

Alhidaaya.com

 

عن أنس بن مالك رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَا بَالُ أقْوامٍ يَرْفَعُونَ أبْصَارَهُمْ إِلَى السَّمَاءِ في صَلاَتِهِمْ ! )) فَاشْتَدَّ قَولُهُ في ذَلِكَ حَتَّى قَالَ :(( لَيَنْتَهُنَّ عَنْ ذَلِكَ ، أَوْ لَتُخطفَنَّ أَبْصَارُهُمْ ! )) .  رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wana nini watu wanaonyanyua macho yao juu mbinguni wakiwa katika Swalaah zao." Akawa mkali na kuwaonya wasifanye hivyo mpaka akasema: "Wakome kufanya hivyo au watapofolewa macho yao." [Al-Bukhaariy]

 

 

Share