13-Malaika: Malaika Wameumbwa Kutokana Na Nuru

 

Malaika

 

Alhidaaya.com

 

13:  Malaika Wameumbwa Kutokana Na Nuru

 

 

Toka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

 "خُلِقَتِ الْمَلاَئِكَةُ مِنْ نُورٍ، وَخُلِقَ الْجَانُّ مِنْ مَارِجٍ مِنْ نَارٍ، وَخُلِقَ آدَمُ مِمَّا وُصِفَ لَكُمْ‏"

 

“Malaika wameumbwa kutokana na nuru, na majini wameumbwa kutokana na mwako wa moto, na mwanadamu ameumbwa kutokana na kile mlichoelezewa (na Allaah kwenye Qur-aan)”.  [Hadiyth Swahiyh.  Imekharijiwa na Muslim].

 

Ama wakati wa kuumbwa kwao, hili Allaah Pekee ndilo Alijualo.  Lakini lisilo na shaka ni kuwa waliumbwa kabla ya mwanadamu kutokana na Neno Lake Ta’aalaa:

 

 “وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي جَاعِلٌ فِي الْأَرْضِ خَلِيفَةً ۖ قَالُوا أَتَجْعَلُ فِيهَا مَن يُفْسِدُ فِيهَا وَيَسْفِكُ الدِّمَاءَ وَنَحْنُ نُسَبِّحُ بِحَمْدِكَ وَنُقَدِّسُ لَكَ ۖ قَالَ إِنِّي أَعْلَمُ مَا لَا تَعْلَمُونَ

 

“Na pale Rabb wako Alipowaambia Malaika:  Hakika Mimi Nitaweka katika ardhi khalifa.  Wakasema:  Utaweka humo atakayefanya ufisadi humo na kumwaga damu, na hali sisi tunakusabihi kwa Himidi Zako na tunakutukuza kwa Utakatifu Wako?  (Allaah) Akasema:  Hakika Mimi Nayajua zaidi msiyoyajua”.  [Al-Baqarah: 30].

 

Khalifa hapa ni baba yetu Aadam (‘Alayhis Salaam) kwa mujibu wa kauli ya Ibn Mas-‘uwd na Ibn ‘Abbaas.

 

 

Share