Keki Ya Zabibu
Vipimo
Unga wa ngano 2 Vikombe
Siagi 1 Kikombe
Sukari 1 Kikombe
Mayai 6
Vanilla 1 Kijiko
Baking Powder 1 Kijiko cha supu
Zabibu kavu ½ Kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
1. Washa oveni moto wa 350°F.
2. Kwenye bakuli la kuchanganyia keki la machine, saga sukari na siagi hadi ilainike.
3. Kisha tia yai moja moja huku unaendelea kuchanganya.
4. Halafu mimina unga uliochungwa pamoja na baking powder na uchanganye vizuri.
5. Kisha tia vanilla na mwagia zabibu na ukoroge.
6. Kisha umimine katika sufuria ya kiasi ya kupikia keki iliyopakwa siagi.
7. Vumbika kwenye oveni kwa muda wa dakika 35 au hadi iwe tayari.
8. Iache ipowe na itakuwa tayari kuliwa.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
