Katelesi Za Nyama Za Kotmiri

Katelesi Za Nyama Za Kotmiri

Vipimo:

Viazi - 3 LB

Nyama - 1 LB

Unga wa mkate (Breadcrumbs) - 1 kikombe cha chai

Mayai - 2-3

Mafuta ya kukaangia - kiasi

Vipimo Vya Nyama:

Tangawazi na kitunguu saumu(thomu) iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Chumvi - Kiasi

Jeera (Bizari ya pilau ya unga) - 1 kijiko cha chai

Dania (Gilgilani ya unga) - 1 kijiko cha chai

Pilipili manga ya unga - 1 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga - ¼ kijiko cha chai

Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Ndimu au limau - 2 vijiko vya supu

Kotmiri iliyokatwakatwa (chopped) -  Msongo 1 kamili au zaidi yake.

Kitunguu kilichokatwa katwa (chopped) - 1 Kikubwa

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Chemsha Viazi, vikiwiva menya maganda na viponde.
  2. Weka nyama katika sufuria ndogo, ichanganye na vitu vyake vyote isipokuwa kotmiri na vitunguu.
  3. Ipike nyama mpaka ikauke.
  4. Tia Kotmiri na vitunguu viliyokatwakatwa, changanya weka kando.
  5. Chukua viazi viliyopondwa Changanya na hiyo nyama.
  6. Fanya madonge kiasi katika mkono ufanye viduara.
  7. Tayarisha katlesi zote hivyo hadi umalize viazi na nyama.
  8. Weka mafuta katika karai yapate moto sawa sawa.
  9. Chomva katlesi katika mayai uliyoyapiga sawa sawa kisha garagaza katika unga wa mkate (breadcrumbs) na uzikaange mpaka zigeuke rangi.
  10. Epua weka katika karatasi ya inayokunwa mafuta (Kitchen paper) au weka katika chujio zichuje mafuta.
  11. Tayari kuliwa.
Share