Mchanganyiko Wa Mboga Za Kuchoma (Baked)

Vipimo
Viazi 5
Karoti 2
Koliflawa (cauliflower) ½
Brokoli 3 misongo (bunch)
Pilipili mboga ya kijani 1
Pilipili mboga nyekundu 1
Thomu iliyosagwa 1 kijiko cha supu
Pilipili manga iliyosagwa 1 kijiko cha chai
*Kidonge cha supu (stock) 1
Parsley kavu iliyokatwa ndogo ndogo (chopped) 2 vijiko vya supu
Chumvi kiasi
Mafuta ya zaytuni (olive oil) 3 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Menya viazi katakata vipande vya mchemraba (cubes)
- Katakata karoti vipande virefu virefu vya kiasi
- Katakata mapilipili mboga vipande vya kiasi kiasi
- Chambua koliflawa na brokoli
- Tia mafuta katika karai, kaanga thomu kidogo kisha tia chumvi, pilipili manga, epua weka kando.
- Weka kidonge cha supu katika kibakuli kidogo, tia maji ya moto kiasi vijiko 3 vya supu, koroga kipate kuyayuka iwe supu. Tia katika sufuria uliyokaangakia thomu.
- Weka mboga zote katika bakuli kisha mimina mchanganyiko wa thomu na supu uchanganye vizuri.
- Tia katika treya ya kupikia ndani ya oveni. Zipike mboga (bake) kwa moto wa takriban 350°C kwa muda wa dakika 15-20.
- Epua kisha mwagia parsely na uchanganye kisha mimina katika bakuli la kupakulia ikiwa tayari kuliwa kwa aina za mikate.
* kidonge cha supu ikiwa ni chicken stock au beef stock.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


