Mema Na Mabaya Yameumbwa Na Allah?

 

Mema Na Mabaya Yameumbwa Na Allah?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Asalam aleikum,

Je, Allah (swt) Aliumba uzuri (good) na ubaya (evil) ama aliumba uzuri pekee na ubaya unatokea kwa sababu watu wanapotezwa na shetani mpotevu. Tafadhali niongoze

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

Hakika ni kuwa Yeye haulizwi anayoyafanya lakini sisi ndio tutaulizwa kwa yote tunayo yafanya hapa duniani na Atatulipa Pepo kwa mema na kutuadhibu na Moto kwa maovu tunayo yatenda. Allah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Aliumba viumbe, mbingu, ardhi na vitu vyenginevyo. Vitendo vibaya au vizuri vinatokana na ule uhuru tuliopatiwa na Allah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Allah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anatuelezea kuwa Ametupatia viungo vya kutusaidia ili kumuabudu Yeye peke na kumtumikia, kumtii na kumnyenyekea. Anasema:

 

إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا﴿٣﴾

Hakika Sisi Tumemuongoza njia; ima (awe) ni mwenye kushukuru au mwenye kukufuru. [Al-Insaan: 3]

 

Na Anasema Allaah Subhaanahu wa Ta'aalaa tena:

 

أَلَمْ نَجْعَل لَّهُ عَيْنَيْنِ ﴿٨﴾وَلِسَانًا وَشَفَتَيْنِ ﴿٩﴾وَهَدَيْنَاهُ النَّجْدَيْنِ ﴿١٠﴾

Je, kwani Hatukumjaalia macho mawili? Na ulimi na midomo miwili?Na Tukambainishia njia mbili (ya haki na upotofu)? [Al-Balad: 8 – 10]

 

Anatuelezea tena:

 

وَلَقَدْ ذَرَأْنَا لِجَهَنَّمَ كَثِيرًا مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ ۖ لَهُمْ قُلُوبٌ لَّا يَفْقَهُونَ بِهَا وَلَهُمْ أَعْيُنٌ لَّا يُبْصِرُونَ بِهَا وَلَهُمْ آذَانٌ لَّا يَسْمَعُونَ بِهَا ۚ أُولَـٰئِكَ كَالْأَنْعَامِ بَلْ هُمْ أَضَلُّ ۚ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْغَافِلُونَ ﴿١٧٩﴾

Kwa yakini Tumeumba Jahannam kwa ajili ya wengi katika majini na wana Aadam. Wana nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama wanyama, bali wao ni wapotovu zaidi. Hao ndio walioghafilika. [Al-Al'raaf: 179]

 

 

Hivyo, mwanadamu ndiye mwenye kufanya hayo maovu na mazuri.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share