Maandazi Ya Kukandiwa Kwa Maziwa

Maandazi Ya Kukandiwa Kwa Maziwa

 

 

Vipimo

 

Unga - 4 vikombe vya chai

 

Sukari - 1 kikombe cha chai

 

Hamira - 1 kijiko cha chai

 

Samli - 1 kijiko cha chai

 

Maziwa  - 1 ½ kikombe cha chai

 

Hiliki -  kiasi

 

Mafuta ya kukaangia -  kiasi

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika   

  

  1. Changanya unga,  hamira, samli, maziwa, kisha  vuruga na kanda ukandike kiasi.   
  2. Kata madonge manane kisha acha uumuke.     
  3. Ukishaumuka sukuma kila donge ukate vipande vinne. 
  4. Panga kwenye meza tena yaumuke.
  5. Weka mafuta ya kukaangia katika karai na yakaange kwa moto mkali wa kiasi.
  6. Yatoe weka kwenye sahani tayari kwa kuliwa.  

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kuburudika)

 

 

 

 

 

Share