Bajia Za Dengu Na Viazi

Bajia Za Dengu Na Viazi 

 

Vipimo

 

Unga wa dengu - 3 vikombe vikubwa

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Mbatata (kiazi) - 2

Maji baridi - 1 glass

Baking powder - 1 cha chai

Kotmiri  iliyokatwakatwa - 4 -5 Miche

Kitunguu maji  -1

Kitunguu saumu (thomu) ilosagwa au ya unga - 1 kijiko cha chai

Mafuta - 500 ml

 

Namna  Ya  Kutayarisha Na Kupika

 

  1. Menya viazi katakata vipande vidogodogo.
  2. Menya kitunguu katakataka slesi ndogo ndogo kiasi
  3. Katakata (chop) kotmiri
  4. Tia unga wa dengu katika bakuli, changanya pamoja na chumvi na baking powder.
  5. Mimina vitu vyote katika bakuli pamoja na kitunguu thomu ulosaga.
  6. Tia maji ukitumia uma au mchapo wa mkono (usotumia umeme) kuvuruga mchanganyo.
  7. Ukisha kuwa laini bila mavimbo, hakikisha si mzito na si uji sana (mwembamba).
  8. Uwache kwa muda wa robo saa (dakika 15) paka 20.
  9. Weka karai  jikoni au sufuria nzito ndogo, tia mafuta na acha yapate moto sawasawa.
  10. Tumia kijiko cha supu kuteka unga  kutia kwenye mafuta , unapotia hakikisha kipimo chako chote kimelenga mahala au sehemu moja bila ya kutapakaza ili uweze kupata  kidonge .
  11. Utaenedelea hivi kwa kujaza karai nafasi yote zikigeuka rangi ya kuiva, unazigeuza upande wa pili paka umalize zikiwiva kwa rangi nzuri.
  12. Tumia sahani ukiwa umetandaza karatasi za jikoni kuweza kuchuja mafuta baada ya  kuchoma. Kisha badilisha kwenye sahani au bakuli nyengine, tayari kuliwa

 

Kidokezo:

 

Huliwa kwa chatini ya aina yoyote.

 

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

 

 

 

 

 

 

Share