Amehamia Nyumba Mpya Na Kumetokea Moto Baada Ya Usiku Wake Kusomwa Qur-aan, Ni Nini?

 

Amehamia Nyumba Mpya Na Kumetokea Moto

Baada Ya Usiku Wake Kusomwa Qur-aan, Ni Nini?

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Mehamia nyumba mpya imetokezea moto juu ya mlango,  na umetokezea kama  umesa ujiani ndani ya nyumba baada usiku kusomwa kuran, jee unaweza kuniambia kwa nini? nipo katika hofu.

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho

 

Hatuwezi kujua sababu ya moto huo, huenda ikawa ni tatizo la umeme. Hakikisha tatizo hilo halipo. Usijitie wasiwasi sana, inatosheleza ukiwa utasoma Qur-aan na nyiradi za asubuhi na jioni na nyinginezo kujiepusha na kila shari na balaa. Bonyeza viungo vifuatavyo upate du'aa za kukuhifadhi In shaa Allaah.

 

Hiswnul-Muslim: Du’aa Na Adhkaar Kusoma Na Kwa Kusikiliza (Toleo Lilohaririwa)

 

027-Hiswnul-Muslim: Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni

 

128-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuzuia Vitimbi Vya Mashaytwaan

 

 

Kisha soma Swali na Jibu lifuatalo upate maelezo ya kuhamia katika nyumba mpya lenye du'aa na nyiradi za kusoma:

 

Unapohamia Katika Nyumba, Unatakiwa Usome Au Kufanya Chochote 

 

Tunakuombea kila la kheri katika nyumba yako mpya, kheri na Baraka.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

  

 

Share