Skip navigation.
Home kabah

Buns Za Nyama Aina Ya 2

 

Vipimo

Mayai                             4

 
Mafuta                             1 kikombe


Maziwa                            1kikombe


Chumvi                            kiasi


Hamira                            1 1/2 kijiko cha supu


Unga                               kiasi

 
Habat suda( blackseed)    1 kijiko cha supu


Nyama yakima  kiasi  ipike kama ya sambusa


Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

1.    
Kwenye  chombo kikubwa changanya mayai, mafuta, maziwa, chumvi changanya vizuri

2.    
Tia hamira na habat suda kisha mimina unga kidogo kidogo mpaka mchanganyiko ushikane uwe laini .

3.    
Iwache  ifure,ukisha fura kata madonge ya kiasi ujaze nyama katikati  kisha ufunge  iwe duwara  panga  kwenye sinia  kisha yapake maziwa kwa juu

4.    
Choma  kwa moto wa 350  mpaka  zibadilike rangi na yawive  vizuri .

5.     Iwache ipoe  kisha  itakuwa tayari kuliwa .


Kidokezo: unaweza kujaza feta cheese na zaituni badala ya nyama  pia inakuwa nzuri .