Skip to main content

Buns Tamu Za Ufuta Na Malai Chungu (sour Cream)

Mikate-Mahamri

Buns Tamu Za Ufuta Na Malai Chungu (sour Cream)

Vipimo

Unga - 4 Vikombe

Sukari -  1 Kijiko cha supu

Chumvi - 1 Kijiko cha chai

Hamira - 1 Kijiko cha supu

Baking powder - 1 Kijiko cha chai

Siagi - ¼ Kikombe

Maziwa -  1 ½ Vikombe

Malai chungu (sour cream) - 2 Vijiko vya supu                                 

Ufuta - Kiasi ya kunyunyizia juu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Katika bakuli changanya vipimo vyote isipikuwa ufuta.
  2. Kisha ukande unga huku unanyunyizia unga ukiwa unashika.
  3. Funika mchanganyiko na weka pahali penye joto hadi iimuke.
  4. Halafu fanya viduara na viweke kwenye treya ya kuchomea iliyopakwa siagi.
  5. Ziache pahali penye joto hadi zimuuke kwa mara ya pili.
  6. Washa oveni moto wa 350°.
  7. Pakiza (brush) Yai uliopiga au maziwa juu ya vile vidonge kisha nyunyizia ufuta juu.
  8. Kisha vumbika kwenye oveni kwa muda wa dakika 15 hivi na kuweka moto wa juu hadi ziive na kugeuka rangi na zitakuwa tayari kuliwa.