Aayah Gani Zinazungumzia Ribaa Katika Biblia?
SWALI:
Assalaamu alaykum warahmatullah
Tafadhali nakuombeni munipatie aya ndani ya Bibilia zinazozungumzia mikopo na riba,
Jazaakallahul khair
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kupatiwa mistari katika Biblia inayozungumzia kuhusu mikopo na Ribaa.
Mwanzo tuanze na Qur-aan inavyosema kuhusu kukatazwa kwa Mayahudi kuchukua RibaA. Allaah Aliyetukuka Anasema:
“Na kuchukua kwao Ribaa, nao wamekatazwa, na kula kwao
Ama katika Biblia zipo aya mbili katika vitabu tofauti, moja ikikataza kuchukua Ribaa kwa maskini na nyingine ikitoa ruhusa kuchukua Ribaa kwa asiyekuwa Muisraili. Hizi ni baadhi ya hizo aya:
1. “Ukimkopesha fedha mtu yeyote miongoni ma watu wangu walio maskini, usiwe kwake
2. “Unaweza kutoza riba unapomkopesha mgeni, lakini ndugu yako Mwisraeli usimtoze riba, naye Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, atakubariki katika shughuli zako zote utakazofanya katika nchi ambayo unakwenda kuimiliki” (Kumbukumbu la Sheria 23: 20).
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha

Assalaamu alaykum, sina
Assalaamu alaykum,
sina comment ila ningependa kujua jinsi ya kutuma maswali katika tovuti hii ili nifahamu mengi nisiyoyajua katika ulimwengu huu wa kiislamu,
Wabillahi tawfiq
Walaykum Salam
Walaykum Salam Warahmatullahi Wabarakatuh.
Ukitaka kutuma maswali kwenye tovuti ya Alhidaaya, basi unatakiwa kutuma ujumbe wako kwenye anuani ifuatayo: maswali@alhidaaya.com
InshaAllah natumai utafaidika ndugu Muislamu.
Kila la kheri