Kuoa Dada Wawili Kwa Pamoja Inajuzu?

Kuoa Dada Wawili Kwa Pamoja Inajuzu?

 

 Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI

 

Assalam alaikum.

Naomba mniweke wazi katika sheria hivi ndugu halisi wa bibi yangu mfano bibi yangu anaitwa raya issa ndugu yake anaitwa salma issa jee itajuzu yaani inafaa kumuowa huyu ndugu yake yaani salma issa ahsante?

 

 

JIBU: 

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

 

Uislamu ni Dini ambayo ina Shariy’ah iliyo sambamba na maumbile ya mwana-Aadam na hakuna jambo lolote isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametuelezea. Hivyo, katika mas-ala ya ndoa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametuwekea wazi wale ambao unaweza kuwaoa na wale ambao huwezi kuwaoa. Na katika usiyeweza kumuoa ni dada ya bibi yako (mkeo). Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

 

حُرِّمَتْ عَلَيْكُمْ أُمَّهَاتُكُمْ وَبَنَاتُكُمْ وَأَخَوَاتُكُمْ وَعَمَّاتُكُمْ وَخَالَاتُكُمْ وَبَنَاتُ الْأَخِ وَبَنَاتُ الْأُخْتِ وَأُمَّهَاتُكُمُ اللَّاتِي أَرْضَعْنَكُمْ وَأَخَوَاتُكُم مِّنَ الرَّضَاعَةِ وَأُمَّهَاتُ نِسَائِكُمْ وَرَبَائِبُكُمُ اللَّاتِي فِي حُجُورِكُم مِّن نِّسَائِكُمُ اللَّاتِي دَخَلْتُم بِهِنَّ فَإِن لَّمْ تَكُونُوا دَخَلْتُم بِهِنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ وَحَلَائِلُ أَبْنَائِكُمُ الَّذِينَ مِنْ أَصْلَابِكُمْ وَأَن تَجْمَعُوا بَيْنَ الْأُخْتَيْنِ إِلَّا مَا قَدْ سَلَفَ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٢٣﴾

Mmeharamishiwa (kuwaoa) mama zenu, na mabinti zenu, na dada zenu, na shangazi zenu, na makhalati zenu (mama wakubwa na wadogo), na mabinti wa kaka, na mabinti wa dada, na mama zenu ambao wamekunyonyesheni, na ndugu zenu kwa kunyonya, na mama wa wake zenu, na watoto wenu wa kambo walio katika ulinzi wenu waliozaliwa na wake zenu ambao mmewaingilia. Lakini ikiwa hamkuwaingilia basi hakuna dhambi (kuwaoa). Na (mmeharamishwa) wake wa watoto wenu waliotoka katika migongo yenu, na kuwaoa dada wawili kwa wakati mmoja, isipokuwa yaliyokwisha pita. Hakika Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nisaa: 23]

 

 

 

Kwa ajili hiyo huwezi ki- Shariy’ah kumuoa Raya binti Issa na dada yake Salma binti Issa, lakini ikiwa Raya ataaga dunia au utamuacha unaweza kumuoa dada yake wakati huo.

 

Na Allah Anajua zaidi

 

Share