100 - Al-'Aadiyaat

 

  الْعَادِيَات

 

100-Al-‘Aadiyaat

 

100-Al-‘Aadiyaat: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com 

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

 

وَالْعَادِيَاتِ ضَبْحًا ﴿١﴾

1. Naapa kwa (farasi) waendao mbio za kasi wakipumua.

 

 

فَالْمُورِيَاتِ قَدْحًا ﴿٢﴾

2. Kisha Naapa kwa wenye kutoa cheche za moto (kwa msuguano wa kwato zao chini).

 

 

فَالْمُغِيرَاتِ صُبْحًا ﴿٣﴾

3. Wenye kushambulia asubuhi.

 

 

فَأَثَرْنَ بِهِ نَقْعًا ﴿٤﴾

4. Huku wakitimua wingu la vumbi kubwa.  

 

 

فَوَسَطْنَ بِهِ جَمْعًا ﴿٥﴾

5. Kisha wakapenya katikati ya kundi (la maadui).

 

 

إِنَّ الْإِنسَانَ لِرَبِّهِ لَكَنُودٌ ﴿٦﴾

6. Hakika binaadamu kwa Rabb wake bila shaka ni mtovu mno wa shukurani.   

 

 

وَإِنَّهُ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٌ ﴿٧﴾

7. Na hakika yeye juu ya hayo bila shaka mwenyewe ni shahidi.

 

 

وَإِنَّهُ لِحُبِّ الْخَيْرِ لَشَدِيدٌ ﴿٨﴾

8. Na hakika yeye ni mwingi mno wa kupenda mali.

 

 

أَفَلَا يَعْلَمُ إِذَا بُعْثِرَ مَا فِي الْقُبُورِ ﴿٩﴾

9. Je, hajui vitakapopinduliwa juu chini na kutolewa vile vilivyomo makaburini?

 

 

وَحُصِّلَ مَا فِي الصُّدُورِ ﴿١٠﴾

10. Na yatapodhihirishwa yale yaliyomo vifuani?

 

 

إِنَّ رَبَّهُم بِهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّخَبِيرٌ ﴿١١﴾

11. Hakika Rabb wao Siku hiyo kwao, bila shaka Ni Mjuzi wa Khabari za dhahiri na siri.

 

 

Share