Imaam Ibn Baaz: Kuendelea Kuishi Na Mke Asiyeswali

Kuendelea Kuishi Na Mke Asiyeswali

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Ni ipi hukmu ya mke asiyeswali, kwa kutambua kuwa nimeshambainishia adhabu anayopata mwenye kuacha kuswali, kuna baadhi ya nyakati anaswali na wakati mwengine anaacha. Kwa mfano anaswali Adhuhuri na anaacha (Swalaah) zote za Faradhi zilizobaki?

 

 

JIBU:

 

Hukmu yake ni Kafiri.

Na haijuzu kuendelea kubaki naye katika hifadhi yako. Inapasa kuwa naye mbali, isipokuwa kama atatubu tawbah ya kweli, la sivyo, ni waajib kuwa naye mbali (kuachana naye).

Kwa sababu kuacha Swalaah ni ukafiri mkubwa.

 

Anasema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

“Baina ya mtu na baina ya ushirikina na ukafiri ni kuacha Swalaah.” [Muslim]

 

Na anasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

“Agano (Kinachotutofautisha) baina yetu (Waumini) na baina yao (Washirikina, Makafiri na Wanafiki) ni Swalaah, anayeiacha (Swalaah) amekufuru.” [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na An-Nasaaiy]

 

Hii ndio kauli sahihi katika kauli za Wanachuoni; kwamba kuiacha (Swalaah) ni ukafiri mkubwa.

 

 

[http://www.binbaz.org.sa/noor/3633]

 

 

 

 

Share