Imaam Ibn Kathiyr: Shariy’ah Ya Dini Imekamilika

Shariy’ah Ya Dini Imekamilika

 

Imaam Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

Imaam Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah) amesema:

 

Shariy’ah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni shariy’ah iliyokamilika kabisa, haikuacha jambo lolote jema lililojulikana na werevu isipokuwa ameliamrisha. Na hakuacha jambo lolote lillilokua ovu na ambalo limejulikana na werevu isipokua amelikataza. Hakuamrisha jambo na watu wakasema "Laiti kama asingeliamrisha". Na Hakukataza jambo wata wakasema "Laiti kama asingelikataza"

 

[Al-Bidaayah Wan-Nihaayah (6/79)]

Share