Ukumbusho Wa Kukithirisha Swawm Mwezi wa Al-Muharram Na Swiyaam Ya Taasu'aa na 'Aashuraa (9 na 10 Al-Muharram) Pamoja Na Masiku Mengineyo

 

Al-Muharram 

 

Ukumbusho Wa Kukithirisha Swiyaam (Funga) Za Mwezi wa Al-Muharram

Na Swiyaam Ya Taasu'aa na 'Aashuraa  (9 na 10 - Al-Muharram) Pamoja Na Masiku Mengineyo

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: 

 أَفْضَلُ الصِّيَامِ بَعْدَ رَمَضَانَ شَهْرُ اللَّهِ الْمُحَرَّمُ  رواه مسلم

"Swiyaam (funga) bora kabisa baada ya Ramadhwaan ni swawm ya mwezi wa Allaah wa Al-Muharram." [Muslim]

 

Tunawanasihi hali kadhalika kufunga siku ya Taasu'aa na 'Aashuraa (Tarehe 9 na 10 Al-Muharram) Asiyeweza Swawm tarehe 9 Al-Muharram basi baadhi ya 'Ulamaa wanasema kuwa mtu anaweza kufunga tarehe 10 na 11 Al-Muharram japokuwa hakuna Hadiyth sahihi ya kufunga siku ya baada yake; yaani Muharram 11. Na asiyejaaliwa kuunganisha Swawm tarehe 9 pamoja na tarehe 10 au kuunganisha Swawm tarehe 10 pamoja na 11 Al-Muharram, basi asikose Swawm ya tarehe 10 Al-Muharram pekee. Hayo ni kutokana na fadhila zake za kufutiwa madhambi ya mwaka mmoja kama ilivyothibiti katika Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

((صِيَامُ يَوم عاشوراء إنِّي أحْتَسبُ علَى اللهِ أن يُكفِّرَ السَّنةَ التِي قبلَه)) رواه مسلم

"Swawm ya siku ya 'Ashuraa, nategemea kutoka kwa Allaah Ayafute madhambi ya mwaka uliotangulia." [Muslim]

 

Kwa faida zaidi soma makala katika kiungo kifuatacho:

 

Fadhila Za Mwezi Wa Al-Muharam Na Siku Ya 'Aashuraa Na Bid'ah Zake

 

Masiku mengineyo ya Swiyaam za Sunnah na fadhila zake:

 

Jumatatu na Alkhamiys:    

 

عن أبي هريرة رضي الله عنه: تُعرَضُ الأعمالُ يومَ الاثنينِ والخميسِ فأحبُّ أن يُعرَضَ عملي وأنا صائمٌ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “'Amali zinapandishwa siku ya Jumatatu na Alkhamiys, basi napenda kwamba zipandishwe 'amali zangu nikiwa mimi niko katika Swawm.” [Swahiyh At-Tirmidhiy 747, Swahiyh At-Targhiyb 1041]

 

Swiyaam ya Jumatatu:

 

عَنْ أَبِي قَتَادَةَ الْأَنْصَارِيِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سُئِلَ عَنْ صَوْمِ الِاثْنَيْنِ فَقَالَ: (( فِيهِ وُلِدْتُ وَفِيهِ أُنْزِلَ عَلَيَّ)) .

Kutoka kwa Abuu Qataadah Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu Swawm ya Jumatatu akasema: “Nimezaliwa siku hiyo na siku hiyo nimeteremshiwa (Qur-aan).” [Muslim]

 

 

Ayyaamul-Biydhw (Tarehe 13, 14, 15)

 

 

Swawm Ya Nabiy Daawuwd:  Siku Kufunga Na Siku Kuacha kutokana na Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

أَحَبُّ الصِّيَامِ إِلَى اللَّهِ صِيَامُ دَاوُدَ، كَانَ يَصُومُ يَوْمًا وَيُفْطِرُ يَوْمًا

"Swawm inayopendeza zaidi kwa Allaah ni Swawm ya Daawuwd, alikuwa anafunga siku moja na anakula siku moja” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida za fadhila za Swiyaam:

 

Fadhila Za Swiyaam Za Fardhi Na Za Sunnah

 

 

Tutaweka taarifa za kuandama mwezi In Shaa Allaah.  

Share