Al-Lajnah Ad-Daaimah: Ramadhwaan: Hakuweza Kulipa Swawm Zilopita Kwa Sababu Ya Uzazi

 

Hakuweza Kulipa Swawm Za Ramadhwaan Zilopita Kwa Sababu Alikuwa Anazaa Siku Za Ramadhwaan

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Nini hukmu kuhusu mwanamke aliyekuwa akizaa siku za Ramadhwaan (kwa kutokea hivyo) muda wa miaka michache na hakuweza kulipa Swawm ya siku alizokuwa hakufunga?

 

 

JIBU:  

 

Inawajibika kwa mwanamke aliyejifungua katika mwezi wa Ramadhwaan kulipa siku alizokuwa hakuweza kufunga siku za mbele.

 

Na ikiwa hakulipa siku hizo bila sababu inayokubalika katika Shariy’ah ya Kiislamu hadi imeingia Ramadhwaan nyingine, basi inampasa  alishe maskini kwa idadi ya siku alizokuwa hakufunga na pia afunge Swawm za siku hizo. 

 

Lakini kama kuchelewa kulipa kulikuwa kwa sababu inayokubaliwa katika Shariy’ah ya Kiislamu basi inamtosha kuzilipa tu siku hizo.

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

[Fataawa Ramadhwaan - Mjalada (2), Ukurasa (588), Fatwa Namba (573);
Fataawa Al-Lajnah Ad-Daaimah lil-Buhuwth Al-'Ilmiyyah wal-Iftaa. - Fatwa Namba (9861)]

 

 

Share