23-Fadhila Za Laa Ilaaha Illa-Allaah: Unapohangaika Kupata Usingizi Sema: Laa ilaaha illa-Allaahul-Waahidul-Qahhaar...

 

Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah

 

www.alhidaaya.com

 

23-Unapohangaika Kupata Usingizi Sema Laa ilaaha illa-Allaahul-Waahidul-Qahhaar..

 

 

عن عائشة أم المؤمنين رضي الله عنها ان رسولُ اللهِ صلَّى اللهُ عليه وسلَّم إذا تضوَّر مِن اللَّيلِ قال: ((لا إلهَ إلَّا اللهُ الواحدُ القهَّارُ ربُّ السَّمواتِ والأرضِ وما بينَهما العزيزُ الغفَّارُ))

 

Imepokelewa kutoka kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipokuwa akihangaika kupata usingizi usiku akisema:

 

لا إِلـهَ إِلاّ اللهُ الـواحِدُ القَهّـار، رَبُّ السَّـمواتِ وَالأرْضِ وَما بَيْـنَهـما، العَزيـزُ الغَـفّار

Laa ilaaha illa-Allaahul-Waahidul-Qahhaar. Rabbus-samawaati wal ardhwi wamaa baynahumaal-’Aziyzul-Ghaffaar.

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah  Al-Waahid (Mmoja Pekee) Al-Qahhaar (Mshindi Mwenye kudhibiti na kudhalilisha). Rabb wa mbingu na ardhi na vilivyo kati yake, Al-’Aziyz (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika daima) Al-Ghaffaar (Mwingi wa kughufuria)) [An-Nasaaiy katika As-Sunan Al-Kubraa (10700), Swahiyh Ibn Maajah (5530), Swahiyh Al-Jaami’ (4693), Al-Haakim na ameisahihisha Adh-Dhahabiy (1/540), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah (864) na Ibn As-Sunniy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah (757)]

 

 

Share