02-Al-Lajnah Ad-Daaimah: Kufanya Hajj Akiwa Bado Ana Deni La Benki

 

 

Kufanya Hajj Akiwa Bado Ana Deni La Benki

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Muislamu alitaka kutekeleza fardhi ya Hajj akiwa ana deni. Je, akiwa ameomba ruhusa kwa wenye kumdai na wamemruhusu kutekeleza Hajj itakuwa imekubaliwa?

 

JIBU:

 

Ikiwa hali ni kama ulivyotaja, kuwa na ruhusa ya wenye kumdai atekeleze Hajj kabla ya kulipa deni, basi hakuna ubaya kufanya Hajj kabla ya kumaliza deni na Hajj haitoathirika (kuwa ina kasoro) kwa kutokana na hali yake ilivyo baina yake na waliomkopesha.

 Na kwa Allah ndio yako mafanikio yote na Rahma na Amani zimfikie Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam na Swahaba zake.

 

 

 

 

[Fataawa al-Lajnah ad-Daaimah lil-Buhuwth al-'Ilmiyyah wal-Iftaa. Mjalada 11, Uk. 46, Fatwa Namba 5545  Imejumuisha:

Kiongozi Mkuu: Shaykh 'Abdul 'Aziyz ibn 'Abdillaah ibn Baaz

Msaidizi Kiongozi Mkuu: Shaykh ‘Abdur-Razzaaq 'Afiyfiy

Mjumbe: Shaykh 'Abdullaah Ibn Ghudayyaan

Mjumbe: Shaykh 'Abdullah ibn Qu'uwd]

 

 

 

 

Share