29-Fadhila Za Laa Ilaaha Illa-Allaah: Allaahumma Inniy As-alauka Bianna Lakal-Hamdu... (Du’aa Hutakabaliwa Kwa Kutajwa Jina Adhimu Kabisa La Allaah)

 

Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah

www.alhidaaya.com

 

29-Allaahumma Inniy As-alauka Bianna Lakal-Hamdu Laa Ilaaha Illa Anta… (Du’aa Hutakabaliwa Kwa Kutajwa Jina Adhimu Kabisa La Allaah)

 

 

عَنْ أَنَسٍ أَنَّهُ كَانَ مَعَ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ جَالِسًا وَرَجُلٌ يُصَلِّي ثُمَّ دَعَا: "اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ بِأَنَّ لَكَ الْحَمْدُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ الْمَنَّانُ بَدِيعُ السَّمَوَاتِ وَالْأَرْضِ يَا ذَا الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ يَا حَيُّ يَا قَيُّومُ"  فَقَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ : ((لَقَدْ دَعَا اللَّهَ بِاسْمِهِ الْعَظِيمِ الَّذِي إِذَا دُعِيَ بِهِ أَجَابَ وَإِذَا سُئِلَ بِهِ أَعْطَى))

 

Imetoka kwa Anas bin Maalik Maalik  (رضي الله عنه)   kwamba alikuwa amekaa pamoja na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)   na mtu mmoja alikuwa akiswali akaomba:

 

اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ بِأَنَّ لَكَ الْحَمْدُ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ الْمَنَّانُ بَدِيعُ السَّمَوَاتِ وَالْأَرْضِ يَا ذَا الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ يَا حَيُّ يَا قَيُّومُ

 

Allaahumma inniy as-aluka bianna Lakal-Hamdu laa ilaaha illaa Anta Al-Mannaanu Badiy’us-samaawaati wal-ardhwi, yaadhal-Jalaali wal Ikiraami, yaa Hayyu yaa Qayyuwmu,  

 

Ee Allaah hakika mimi nakuomba, kwa vile Himdi ni Zako, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, Mwingi wa Kuneemesha,  Mwanzishi wa mbingu na ardhi, Ee Mwenye Ujalali na Ukarimu, Ee Uliyehai daima, Msimamizi wa kila kitu.   

 

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((kwa yakini amemuomba Allaah kwa Jina Lake Tukufu ambalo Anapoombwa kwalo Anaitikia na Anapotakwa kwalo jambo hutoa)) - Ahlus-Sunan; Abu Daawuwd [1495], An-Nasaaiy (3/52), ibn Maajah [3858] na taz Swahiyh ibn Maajah (2/329)

 

 

Share