Skip to main content

Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah

www.alhidaaya.com

43-Jambo La Kwanza Kuwalingania Makafiri Kuingia Katika Uislamu

Liwe Ni Laa Ilaaha Illa-Allaah

 عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  لَمَّا بَعَثَ مُعَاذًا إِلَى الْيَمَنِ: قَالَ لَهُ: ((إِنَّكَ تَأْتِي قَوْمًا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ، فَلْيَكُنْ أَوَّلَ مَا تَدْعُوهُمْ إِلَيْهِ شَهَادَةَ أَن لاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ)) وَفِي رِوَايَةٍ: ((إِلَى أَنْ يُوَحِّدُوا اَللَّهَ. فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوكَ لِذَلِك فَأَعْلِمْهُمْ أَنَّ اَللَّهَ اِفْتَرَضَ عَلَيْهِمْ خَمْسَ صَلَوَاتٍ فِي كُلِّ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ. فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوكَ لِذَلِكَ فَأَعْلِمْهُمْ أَنَّ اَللَّهَ اِفْتَرَضَ عَلَيْهِمْ صَدَقَةً تُؤْخَذُ مِنْ أَغْنِيَائِهِمْ فَتَرُدُّ عَلَى فُقَرَائِهِمْ. فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوكَ لِذَلِكَ فَإِيَّاكَ وَكَرَائِمَ أَمْوَالِهِمْ, وَاتَّقِ دَعْوَةَ الْمَظْلُومِ فَإِنَّهُ لَيْسَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ اَللَّهِ حِجَابٌ)) أَخْرَجَاهُ

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipomtuma Mu’aadh Yemen alimwambia: ((Hakika wewe utakutana na watu miongoni mwa Ahlul-Kitaab, basi jambo la kwanza la kuwalingania liwe ni kushuhudia kwamba: Laa ilaaha illa-Allaah - hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah)). Na katika riwaayah nyingine: (([Walinganie] Kumpwekesha Allaah. Watakapokutii hilo, wajulishe kwamba Allaah Amewafaradhishia Swalaah tano usiku na mchana. Watakapokutii hilo, basi wajulishe kwamba Allaah Amewafaradhishia Zakaah ichukuliwe kutoka kwa matajiri wao na kupewa masikini wao. Watakapotii hilo, basi tahadhari kuchukua bora za mali zao [kama malipo ya Zakaah], na tahadhari na du’aa ya aliyedhulumiwa, kwani hakuna kizuizi baina yake na Allaah)) [Al-Bukhaariy (1395) Muslim (19)]