044-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Twahara: Yanayotengua Kupukusa

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Twahara

 

044-Yanayotengua Kupukusa

 

Alhidaaya.com

 

 

Imetangulia katika Hadiyth iliyoelezewa na Swafwan bin ‘Assal akisema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi waalihi wa sallam), alikuwa akituamuru tunapokuwa safarini, tusizivue khufu zetu siku tatu na masiku yake ila kwa janaba, lakini si kwa kwenda haja kubwa, au ndogo, au kulala”.

 

Kwa Hadiyth hii, imejulikana kuwa haifai kupukusa juu ya khufu mbili linapotokea moja kati ya mambo yafuatayo:

 

1- Janaba na mengineyo yenye kuwajibisha kuoga kama vile kujitwaharisha na hedhi au nifasi.

 

2- Kumalizika muda wa kupukusa.

 

3- Kuivua khufu na kupata hadathi kabla ya kuivaa.

 

Endapo ataivua khufu yake - ijapokuwa kabla ya kumalizika muda – kisha akapata hadathi, basi haitojuzu kuivaa na kupukusa, kwani anakuwa hakuivaa wakati huo akiwa na twahara.

 

Kwa hivyo, kama litatokea lolote kati ya mambo haya matatu, haitojuzu kupukusa juu ya khufu mbili, bali linalopasa kwake anapopata hadathi, ni kutawadha na kuosha miguu yake miwili, kisha anaweza kuzivaa khufu zake na kupukusa juu yake kama ilivyotangulia.

 

 

Share