051-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Twahara: Niya Ni Sharti Ya Kusihi Kukoga

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Twahara

 

051-Niya Ni Sharti Ya Kusihi Kukoga

 

Alhidaaya.com

 

 

Hii ni kwa vile kukoga ni ‘ibaadah isiyojulikana ila kupitia sharia, na kwa ajili hiyo, niya imekuwa ni sharti humo. Niya yenyewe, ni moyo kuazimia tendo la kukoga ikiwa ni kufuata na kuitii Amri ya Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam). Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa) Anasema:

((وما أمروا إلا ليعبدوا الله مخلصين له الدين))

((Na hawakuamrishwa ila kwa ajili ya kumwabudu Allaah wakimtakasia Yeye Dini)). [Al-Bayyinah (98:5)]

 

Ikhlaasw ni kusudio la kujikurubisha kwa Allaahu (Subhaanahuu Wata'alaa) na kumwelekea Yeye tu katika kutekeleza yale Aliyoyafaradhisha kwa Waja Wake Waumini.

Na Rasuli (Swalla Allaahu 'Alayhi Waalihii Wasallam) anasema:

((إنما الأعمال بالنيات))

((Hakika amali ni kwa niya)).[Hadiyth Swahiyh: Imekwishatajwa].

Na hili la kukoga ni amali. [Angalia Mlango wa ((Niya Ni Sharti Ya Kuswihi Wudhuu uk.40))].

 

 

Share