061-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Twahara: Usharia Wa Kutayammamu

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Twahara

 

061-Usharia Wa Kutayammamu

 

Alhidaaya.com

 

 

Kutayamamu kumethibiti katika Qur-aan, Hadiyth na Ijma’a.

 

1- Katika Qur-aan, ni Neno Lake Allaah Mtukufu:

((فلم تجدوا ماء فتيمموا صعيدا طيبا))

((na hamkupata maji, basi tayamamuni kwa vumbi lililo safi)). [Al-Maaidah (5:6)]

 

2- Katika Hadiyth, ni neno lake Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam):

((جعلت الأرض كلها لي ولأمتي مسجدا وطهورا، فأينما أدركت رجلا من أمتي الصلاة، فعنده مسجده وعنده طهوره))

(( Ardhi yote imefanywa kwangu na kwa umati wangu kuwa ni sehemu ya kuswalia na kujitwaharishia. Na popote itakapomkuta Swalaah yeyote katika umma wangu, basi hapo ndipo pake pa kuswalia na pake pa kujitwaharisha)). [Hadiyth Hasan: Imefanyiwa “ikhraaj” na Ahmad (2/222) kupitia ‘Amri bin Shu’ayb toka kwa babaye toka kwa babuye].

 

Na Hadiyth ya ‘Imraan bin Haswiyn, amesema:

“ Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) aliswali, kisha akamwona mtu mmoja kajitenga kando hakuswali na wengine. Akamwambia:

((يا فلان، ما منعك ألا تصلي مع القوم؟))

(( Ee fulani! Una nini usiswali na watu?)) Akajibu: “Ee Rasuli wa Allaah! Nimepata janaba na maji hakuna”. Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) akamwambia:

((عليك بالصعيد فإنه يكفيك))

((Tumia vumbi, kwani linakutosheleza)).

Maji yalipopatikana, Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihii wa sallam) alimpa mtu huyo chombo cha maji akamwambia:

((اغتسل به))

(( Ogea)). [Hadiyth Swahiyh: Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaariy (348) na Muslim (1535)].

 

3- Ama Ijma’a, Ibn Qudaamah katika Al-Mughniy (1/148) amesema:

“Umma wote kwa jumla umejuzisha kutayamamu”.

 

 

Share