Sambusa Za Kuku Na Mboga

Sambusa Za Kuku Na Mboga

Vipimo

Manda ya sambusa ya tayari Kiasi inavyouzwa - (Kiasi ya sambusa 40-50)

Mafuta ya kukaangia - Kiasi

Kuku (kidari) kilichosagwa - 1 Kilo

Kitunguu saumu(thomu) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chai

Pilipili manga - 1 kijiko cha supu

Bizari ya pilau ya unga (cummin powder) - 1 kijiko cha chai

Bizari ya mchuzi - 1 kijiko cha chai

Ndimu - 1 kijiko cha supu

Mboga mchanganyiko (za barafu) - 1 kikombe                 

Chumvi - Kiasi

Nyanya iliyokatwa ndogo ndogo - 1

Vitunguu maji vilivyokatwa (chopped) - 1 Kikombe

Kotmiri iliyokatwa (chopped)

Namna ya kutayarisha na kupika

  1. Pika nyama ya kuku ya kusagwa kwa kutia chumvi,   thomu na tangawizi, pilipili, ndimu na bizari zote.
  2. Karibu na kuwiva tia mboga za mchanganyiko (frozen vegetables).
  3. Zima moto na tia nyanya, vitunguu na kotmiri.
  4. Funga sambusa katika manda kama kawaida.
  5. Pika sambusa katika mafuta ya moto hadi ziwe nyekundu na zikiwa tayari kuliwa.

 

 

 

 

Share