03-Hadiyth Husnul-Khuluq: Husnul-Khuluq Inasababisha Miyzaan Ya 'Amali Kuwa Nzito Siku Ya Qiyaamah
Hadiyth: Husnul-Khuluq (Tabia Njema)
Hadiyth Ya 3
Husnul-Khuluq Inasababisha Miyzaan Ya 'Amali Kuwa Nzito Siku Ya Qiyaamah
عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (( مَا مِنْ شَىْءٍ أَثْقَلُ فِي الْمِيزَانِ مِنْ حُسْنِ الْخُلُقِ ))
Imepokelewa kutoka kwa Abuu Ad-Dardaai kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakuna kitakachokuwa kizito katika Miyzaan kama Husnul-Khuluq [tabia njema])) [Sunan Abiy Daawuwd, As-Silsilah Asw-Swahiyhah ((2/535), Swahiyh Al-Jaami’ 7=5721, Swahiyh Adab Al-Mufrad (204)]
