03-Shaykh 'Abdul-'Aziyz Aal Ash-Shaykh: Kupiga Punyeto Mchana Wa Mwezi Wa Ramadhwaan
Kupiga Punyeto Mchana Wa Mwezi Wa Ramadhwaan
Shaykh 'Abdul-'Aziyz Aal Ash-Shaykh (Rahimahu-Allaah)
SWALI:
Muuliza kutoka Canada anauliza, nimetoa Manii (punyeto) mchana wa Ramadhwaan hali ya kuwa nimefunga. Nifanye nini?
JIBU:
(Alichofanya ni haraam) na ni juu yake alipe siku hio. Kwa kuwa kutoa manii kwa makusudi haijuzu. Allaah Anasema: "Mwenye kufunga anatakiwa kuacha chakula chake, kinywaji chake na matamanio yake kwa ajili Yangu".
