Kuku Wa Sosi Tamu (Trinidad)

Kuku Wa Sosi Tamu (Trinidad)

Vipimo    

Kuku -  6 LB

Kitunguu saumu/thomu na tangawizi iliyosagwa - 2 vijiko vya supu

Mtindi (Yoghurt)  - 2 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Pilipili nyekundu ya unga - 1 kijiko cha chai 

Sosi 

Mafuta  - 2 vijiko vya supu

Thomu iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Sosi ya tomato (tomato sauce) - ¼ kikombe

Sosi ya HP - 2 Vijiko vya supu

Cellery - 1 mche

Parsley na kotmiri  -  ¼ kikombe                  

Nyanya - 3  

Chumvi - kiasi

Pilipili manga - 1 Kijiko cha supu 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika 

  1. Mkate kuku vipande vikubwa vikubwa, msafishe kwa siki atoke harufu
  2. Mrowanishe na thomu, tangawizi , chumvi, mtindi na pilipili kwa muda wa  saa au zaidi.
  3. Mtie katika tryea ya kupikia katika oveni.
  4. Mchome kwa moto juu (grill) au ukipenda moto wa chini (bake) , akishawiva pakua katika bakuli la kupakulia.
  5. Tengeneza sosi kwa kufanya ifuatavyo:
  6. Saga kwanza Nyanya, cellery, parsely na kotmiri.
  7. Kaaanga thomu katika mafuta kisha tia sosi zote pamoja na mchanganyiko uliosaga wa cellery.
  8. Mwagia sosi katika kuku akiwa tayari kuliwa. 

Kidokezo :  Nzuri kula na wali kama pilau kavu au upendavyo.  

 

 

Share