Kastadi Ya Biskuti

Kastadi Ya Biskuti


Vipimo

Mayai - 2

Maji - 3 Gilasi

Unga wa ngano - 3 vijiko vya supu

Nido (maziwa ya unga) - 2 gilasi

Sukari -  1/2 - 3/4 gilasi

Bisikuti za kawaida plain

Chocoleti

Vanilla - Kiasi 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Tia maji kwanza kwenye blenda pamoja na hivyo vyote; na iache ichanganyikane vizuri.
  2. Kisha tia mchanganyiko kwenye sufuria na tumia mwiko ukoroge moto mdogo na upike mpaka ishikane kama kastadi.
  3. Kisha twaa bakuli utie nusu ya hiyo kastadi upange biskuti kati kati halafu utie nusu nyingine ya hiyo kastadi juu ya hizo biskuti na kisha kwaruzia chokoleti juu yake.
  4. Halafu weka kwenye firiji.                                            
  5. Iache iwe baridi kisha pakuwa kwenye vibakuli na itakuwa tayari kuliwa.

Kidokezo:

 

Inategemea na kipimo cha gilasi kupata saizi ya kastadi.

 

 

Share