031-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuharamishwa kwa Mtu Mwenye Uwezo Kukataa Kulipa Deni

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب تحريم مطل الغني بحقٍّ طلبه صاحبه

031-Mlango Wa Kuharamishwa kwa Mtu Mwenye Uwezo Kukataa Kulipa Deni

 

Alhidaaya.com

 

قال الله تَعَالَى :

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا  ﴿٥٨﴾

Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe. [An-Nisaa: 58]

فَإِنْ أَمِنَ بَعْضُكُم بَعْضًا فَلْيُؤَدِّ الَّذِي اؤْتُمِنَ أَمَانَتَهُ  ﴿٢٨٣﴾

Na ikiwa mmoja wenu amewekewa amana na mwengine, basi airudishe yule ambaye ameaminiwa amana ya mwenzake [Al-Baqarah: 283]

 

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَطْلُ الغَنِيِّ ظُلْمٌ، وَإِذَا أُتْبعَ أَحَدُكُمْ عَلَى مَلِيءٍ فَلْيَتْبَع )) . متفق عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai kwa tajiri kukwepa kulipa deni, ni dhulma. Na mmoja wenu atakaposhawishiwa kwa mwenye uwezo, basi na akubali." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Share