082-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Uharamu wa Mke Kukataa Mwito wa Mumewe Anapomuita Kitandani na Hana Udhuru Wowote wa Kisheria

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب تحريم امتناع المرأة من فراش زوجها

إِذَا دعاها ولم يكن لَهَا عذر شرعي

082-Mlango Wa Uharamu wa Mke Kukataa Mwito wa Mumewe Anapomuita Kitandani na Hana Udhuru Wowote wa Kisheria

 

Alhidaaya.com

 

 

عن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا دَعَا الرَّجُلُ امْرَأتَهُ إِلَى فِرَاشِهِ فَأبَتْ ، فَبَاتَ غَضْبَانَ عَلَيْهَا ، لَعَنَتْهَا المَلاَئِكَةُ حَتَّى تُصْبحَ )) متفق عَلَيْهِ .

وفي رواية : (( حَتَّى تَرْجعَ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapomuita mume, mkewe kwenye firasha (kwa jimai) na asije, hivyo mume kulala akiwa na hasira, mke analaaniwa na Malaaikah mpaka kunapopambazuka." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na katika riwaayah nyengine: "Mpaka atakaporudi (na kumtekelezea mumewe mahitaji yake)." 

 

 

Share