Matunda Mchanganyiko Na Malai

Matunda Mchanganyiko Na Malai 

Vipimo 

Embe- 3

Zabibu -  2 vikombe

Stroberri - 1 kikombe

Shammaam (tikiti cantelope) -  ½

Tikiti la asali  (honey dew)  -  ½

Tofaha (apples) - 2

Peaches - 3

Papayi -  ½

Juisi ya embe - 2 vikombe

Malai (Cream) - 1 kikombe  

Namna Ya Kutayarisha

  1. Menya na katakata matunda yote isipokuwa zabibu utie katika bakuli
  2. Mimina juisi ya embe uchanganye vizuri
  3. Mwagia malai (cream) katikati au tia unapopakua katika vibakli vyake.
  4. Unaweza kulia  pia na iskrimu (ice-cream) upendayo.

Kidokezo:

Unaweza kubadlisha matunda, kuongeza au kupungza upendavyo.  

 

  

 

Share