Ibaadah Zipasazo Kutekelezwa Siku Ya Ijumaa

 

 

 

'Ibaada Zipasazo Kutekelezwa Siku Ya Ijumaa

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

Ijumaa ni siku tukufu kwa Waislamu. ‘Ibaadah kadhaa zenye fadhila adhimu zinapasa kutekelezwa siku hiyo kama ifuatavyo pamoja na dalili zake:

 

  

 

1-Ghuslu (Kuoga)

 

حديث أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ، عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: الْغُسْلُ يَوْمَ الْجُمُعَةِ وَاجِبٌ عَلَى كُلِّ مُحْتَلِمٍ. أخرجه البخاري

 

Kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu)  ambaye alisema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)   amesema: ((Ghuslu (kukoga kwa kujitia twahara) siku ya Ijumaa ni wajibu kwa kila Muislamu aliyebaleghe)) [Al-Bukhaariy]

 

Pia, inapendekezwa kwa kila anayekwenda kuswali kujisafisha, kupiga mswaki, kujitia mafuta mazuri (isipokuwa mwanamke) na kuvaa nguo iliyo nzuri kabisa. Muislamu akitimiza adabu ya Swalaah ya Ijumaa hufutiwa madhambi yake ya wiki.

 

 

عَنْ سَلْمَانَ الْفَارِسِيِّ، قَالَ قَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ لاَ يَغْتَسِلُ رَجُلٌ يَوْمَ الْجُمُعَةِ، وَيَتَطَهَّرُ مَا اسْتَطَاعَ مِنْ طُهْرٍ، وَيَدَّهِنُ مِنْ دُهْنِهِ، أَوْ يَمَسُّ مِنْ طِيبِ بَيْتِهِ ثُمَّ يَخْرُجُ، فَلاَ يُفَرِّقُ بَيْنَ اثْنَيْنِ، ثُمَّ يُصَلِّي مَا كُتِبَ لَهُ، ثُمَّ يُنْصِتُ إِذَا تَكَلَّمَ الإِمَامُ، إِلاَّ غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجُمُعَةِ الأُخْرَى ‏"‏‏.‏  رواه البخاري

 

Kutoka kwa Salmaan Al-Faarisiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muislamu atakayekoga (Ghuslu)  siku ya Ijumaa, akajisafisha vizuri awezavyo, akatia rangi (nywele zake) (isiyo nyeusi),  au akajipaka mafuta mazuri  aliyonayo nyumbani kwake, kisha akaenda Msikitini bila ya kufarikisha (kuwapangua akipita) watu wawili (ambao wameshakaa kitako msikitini), akaswali aliyofaridhishwa, kisha akasikiliza  (khutbah) kimya, hufutiwa madhambi yake yaliyo baina ya Ijumaa hiyo na Ijumaa ijayo.  [Al-Bukhaariy na Ahmad]

 

 

2-Swalaah Ya Ijumaa 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)    Ametuamrisha kwenda kuswali Swalaah ya Ijuma Anaposema:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ وَذَرُوا الْبَيْعَ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴿٩﴾

Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya Swalaah siku ya Ijumaa, kimbilieni kumdhukuru Allaah na acheni kuuza na kununua. Hivyo ni kheri kwenu mkiwa mnajua. [Al-Jumu’ah 62: 9]

 

 

Ni wajibu kwa kila mwanamme Muislamu kwenda kuswali Ijumaa, na hatari ya  kutokwenda kuswali bila ya kuwa na sababu inayoruhusu shariy’ah ni kuwa  Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)   Humpiga muhuri mtu  moyoni  mwake kwa kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

 مَنْ تَرَكَ ثَلاَثَ جُمَعٍ تَهَاوُنًا بِهَا طَبَعَ اللَّهُ عَلَى قَلْبِهِ   -رواه أحمد وأصحاب السنن

 ((Atakayeacha (kuswali Swalaah ya) Ijumaa mara tatu bila ya sababu yeyote, Allaah  humpiga muhuri katika moyo wake))  [Ahmad na wapokezi wa Hadiyth wengine wenye vitabu vya ‘Sunnan’]

 

Kupigwa muhuri huo inamaanisha kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)   Ameshampa chapa huyu mtu kuwa ni 'Aasi na amekwishatumbukia katika makemeo ya Allaah  kwamba   ni katika walioghafilika  kama alivyotutahadharisha Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

ابن عمر وأبي هريرة     أَنَّهُمَا، سَمِعَا رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ عَلَى أَعْوَادِ مِنْبَرِهِ ‏ "‏ لَيَنْتَهِيَنَّ أَقْوَامٌ عَنْ وَدْعِهِمُ الْجُمُعَاتِ أَوْ لَيَخْتِمَنَّ اللَّهُ عَلَى قُلُوبِهِمْ ثُمَّ لَيَكُونُنَّ مِنَ الْغَافِلِينَ ‏"

Kutoka kwa Ibn 'Umar na Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba wamemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Wasiohudhuria  Swalaah ya Ijumaa  wabadilishe  mtindo wao huo au sivyo Allaah  Atawapiga mihuri katika nyoyo zao  na watakuwa  miongoni wa walioghafilika.” [Muslim]

 

 

3-Kufika Mapema Msikitini

 

Kila atakapofika mtu mapema Msikitini huwa amepata daraja fulani na muhimu kabisa ni kufika kabla ya khutba kuanza, akichelewa mtu kufika akakosa khutba atakuwa amekosa Swalaah ya Ijumaa.

 

حديث أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، أَنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: مَنِ اغْتَسَلَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ غُسْلَ الْجَنَابَةِ ثُمَّ رَاحَ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ بَدَنَةً، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الثَّانِيَةِ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ بَقَرَةً، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الثَّالِثَةِ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ كَبْشًا أَقْرَنَ، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الرَّابِعَةِ فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ دَجَاجَةً، وَمَنْ رَاحَ فِي السَّاعَةِ الْخَامِسَةِ فَكَأَنَّما قَرَّبَ بَيْضَةً، فَإِذَا خَرَجَ الإِمَامُ حَضَرَتِ الْمَلاَئِكَةُ يَسْتَمِعُونَ الذِّكْرَ. أخرجه البخاري

 

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: “Atakayekoga (Ghuslu) siku ya Ijumaa kisha akaenda Msikitini, itakuwa kama mfano ametoa (kafara ya) ngamia. Akienda  saa ya pili yake, itakuwa kama katoa (kafara ya) nġ’ombe.  Akienda saa ya tatu yake, itakuwa kama katoa (kafara ya) kondoo mwenye pembe. Akienda saa ya nne yake, itakuwa kama katoa   kuku. Akienda saa ya tano yake itakuwa kama katoa yai. Imaam akifika, Malaika watatoka kuja kusikiliza dhikr” [Al-Bukhaariy]

 

 

4-Kusoma Suwrah Al-Kahf:

 

‘Ulamaa wengi wanaonelea kuisoma Suwratul-Kahf siku ya Ijumaa kutokana na Hadiyth ifuatayo chini, lakini Wanachuoni wa Hadiyth wamesema hakuna Hadiyth iliyothibiti kwa lafdhi ya kuisoma siku ya Ijumaa kama zinavyotaja Hadiyth hizo. Bali ni siku yoyote kama ilivyokuja katika Hadiyth ya mwisho ya mlango huu.

 

Walioonelea inafaa kusomwa Ijumaa, wametolea ushahidi kwa Hadiyth hii:

 

عن أبي سعيد الخدري رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم  قال: من قرأ سورة الكهف يوم الجمعة أضاء له من النور ما بين الجمعتين. رواه الترمذي

 

Kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Atakayesoma Suwratul-Kahf siku ya Ijumaa atakuwa katika mwangaza baina ya Ijumaa mbili.”  [At-Tirmidhiy]

 

Pamoja na kusemwa kuwa Hadiyth hiyo imetoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  lakini Wanachuoni wa Hadiyth wengi wamesema ni Hadiyth 'Mawquuf' ambayo haijaelezwa na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  bali ni kutoka kwa Maswahaba, na kwa nyongeza ya neno 'atakayeisoma Ijumaa' haikuthibiti kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) , na maelezo hayo hapo juu ni ya kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriyy na yeye ndiye aliyekuwa akiisoma Suwrah hiyo katika siku ya Ijumaa, na Wanachuoni wanasema kuwa maadam Maswahaba walikuwa wakiisoma Suwrah hiyo siku ya Ijumaa, basi hakuna neno kuisoma Ijumaa, japo kuisoma siku yoyote ni sawa na mtu atapata fadhila zilizotajwa kwenye Hadiyth hiyo. Ama kutoka kwa  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam),  Wanachuoni wamesema haikuja na lafdhi ya 'kuisoma Ijumaa', bali imekuja kwa ujumla wake wa kuisoma Suwrah hiyo siku yoyote ile kama ilivyokuja hapa chini:

 

قال صلى الله عليه وسلم: ((من قرأ سورة الكهف كما أنزلت كانت له نورا يوم القيامة، من مقامه إلى مكة ، و من قرأ عشر آيات من آخرها ثم خرج الدجال لم يضره...))  صححه الألباني في سلسلة الأحاديث الصحيح 

 Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:  atakayesoma Suwratul-Kahf kama ilivyoteremshwa, atakuwa na mwangaza siku ya Qiyaamah pale alipo mpaka Makkah, na atakayesoma Aayah kumi za mwisho kisha akitokea Dajjaal hatomdhuru)) [Swahiyh kama alivyoeleza Shaykh Al-Albaaniy katika Silsilatul-Ahaadiyth As-Swahiyhah]

 

 

 

5-Suwrah Ya Kusoma Katika Swalaah Ya  Alfajiri

 

حديث أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، قَالَ: كَانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم يَقْرَأُ فِي الْجُمُعَةِ، فِي صَلاَةِ الْفَجْرِ، آلَم تَنْزيلُ، السَّجْدَةَ، وَ هَلْ أَتَى عَلَى الإِنْسَانِ. أخرجه البخاري

 

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye alisema:  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa    akisoma Suwrah ya Alif-Laam-Tanziylu (Suwratus Sajdah) na Hal-Ataa 'Alal-Insaan (Suwratul Insaan)”  [Al-Bukhaariy]

 

 

6-Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa wingi:

 

 

عَنْ أَوْسِ بْنِ أَوْسٍ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ مِنْ أَفْضَلِ أَيَّامِكُمْ يَوْمَ الْجُمُعَةِ، فَأَكْثِرُوا عَلَيَّ مِنْ الصَّلاةِ فِيهِ، فَإِنَّ صَلاَتَكُمْ مَعْرُوضَةٌ عَلَيَّ)) قَالوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَكَيْفَ تُعْرَضُ صَلاتُنَا عَلَيْكَ وَقَدْ أَرَمْتَ؟  قَالَ: يَقُولُ:  بَلِيتَ  قَالَ: ((إِنَّ اللَّهَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى حَرَّمَ عَلَى الأَرْضِ أَجْسَادَ الأَنْبِيَاءِ)) رواه ابو داوُود بِاِسنادٍ صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Aws bin Aws (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Hakika siku zenu zilizo bora mno ni siku ya Ijumaa, basi kithirisheni kuniswalia siku hiyo, hakika Swalaah zenu huwa naletewa)). Maswahaba wakauliza: “Ee Rasuli wa Allaah! Vipi Swalaah zetu kuwa unaletewa na ilihali wakati huo utakuwa umeshaoza?” Akajibu: ((Hakika Allaah Ameiharamisha ardhi kula viwiliwili vya Manabii)).  [Abu

 

 

Pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (( خَيْرُ يَوْمٍ طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ يَوْمُ الْجُمُعَةِ فِيهِ خُلِقَ آدَمُ وَفِيهِ أُدْخِلَ الْجَنَّةَ وَفِيهِ أُخْرِجَ مِنْهَا وَلاَ تَقُومُ السَّاعَةُ إِلاَّ فِي يَوْمِ الْجُمُعَةِ))

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Siku bora kabisa iliyochomoza jua ni siku ya Ijumaa, na hiyo ndio ameumbwa Aadam na hiyo ndio aliingizwa Jannah (Peponi) na akatolewa humo. Na Qiyaamah hakitosimamia siku yoyote isipokuwa siku ya Ijumaa)) [Muslim]

 

 

 

7-Kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) Kwa Wingi Khasa Nyakati Za Jioni:

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ وَذَرُوا الْبَيْعَ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴿٩﴾

Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya Swalaah siku ya Ijumaa, kimbilieni kumdhukuru Allaah na acheni kuuza na kununua. Hivyo ni kheri kwenu mkiwa mnajua.

 

فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّـهِ وَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا لَّعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴿١٠﴾

Na inapomalizika Swalaah, tawanyikeni katika ardhi, na tafuteni katika fadhila za Allaah, na mdhukuruni Allaah sana ili mpate kufaulu.

 

 

وَإِذَا رَأَوْا تِجَارَةً أَوْ لَهْوًا انفَضُّوا إِلَيْهَا وَتَرَكُوكَ قَائِمًا ۚ قُلْ مَا عِندَ اللَّـهِ خَيْرٌ مِّنَ اللَّـهْوِ وَمِنَ التِّجَارَةِ ۚ وَاللَّـهُ خَيْرُ الرَّازِقِينَ﴿١١﴾

Na wanapoona tijara au pumbao wanaikimbilia, na wanakuacha umesimama. Sema: “Yaliyoko kwa Allaah ni bora zaidi kuliko pumbao na tijara, na Allaah ni Mbora wa wenye kuruzuku.   [Al-Jumu’ah (62: 9-11)]

 

 

8-Kuomba Du’aa Khasa Baada Ya Swalaah Ya Alasiri Kwani Ni Wakati Du’aa Inatakabaliwa:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) ذَكَرَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ فَقَالَ:  ((فِيهِ سَاعَةٌ لاَ يُوَافِقُهَا عَبْدٌ مُسْلِمٌ وَهُوَ قَائِمٌ يُصَلِّي يَسْأَلُ اللَّهَ تَعَالَى شَيْئًا إلاَّ أَعْطَاهُ إِيَّاهُ)) وَأَشَارَ بِيَدِهِ يُقَلِّلُهَا

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ametaja Siku ya Ijumaa akasema: ((Humo mna saa haimwafikii mja Muislamu akiwa amesimama anaswali anamwomba Allaah تعالى kitu ila Anampa)). Akaashiria kuonyesha ukaribu wake [Al-Bukhaariy (935), Muslim (852) na wengineo]

 

Rai za ‘Ulamaa kuhusu Saa katika siku ya Ijumaa inayotakabaliwa du’aa zimetajwa nyakati kadhaa, ila waliyokubaliana zaidi yao ni saa ya mwisho kabla ya Swalaah ya Magharibi:

 

 

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ (رضي الله عنه) عَنْ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((يَوْمُ الْجُمُعَةِ اثْنَتَا عَشْرَةَ سَاعَةً ،لاَ يُوجَدُ فِيهَا عَبْدٌ مُسْلِمٌ يَسْأَلُ اللَّهَ شَيْئًا إلاَّ آتَاهُ إِيَّاهُ ، فَالْتَمِسُوهَا آخِرَ سَاعَةٍ بَعْدَ الْعَصْر))

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Siku ya Ijumaa kuna masaa kumi na mbili ambayo hapatikani mja Muislamu anayemwomba Allaah kitu ila Anampa, basi itafuteni baada ya Swalaah ya Alasiri))  [Swahiyh Abiy Daawuwd (1048), Swahiyh An-Nasaaiy (1388), Swahiyh Al-Jaami’ (8190)]

 

 

Share